-
Dumisha Ushikamanifu Ukiwa na Moyo KamiliMnara wa Mlinzi—2008 | Agosti 15
-
-
Nabii Fulani Mzee “Alimdanganya”
8. Ushikamanifu wa nabii wa Mungu ulijaribiwa jinsi gani?
8 Mambo yangemwendea vizuri nabii wa Mungu ikiwa angeendelea na safari yake ya kurudi nyumbani. Hata hivyo, punde tu baadaye, alikabili jaribu lingine. Biblia inasema hivi: “Nabii fulani mzee alikuwa akikaa Betheli, na wanawe wakaja na kumsimulia” mambo yote yaliyotendeka mapema siku hiyo. Anaposikia habari hiyo, mwanamume huyo mzee anawaomba wanawe wamtandikie punda ili amfuate nabii wa Mungu. Punde si punde, anamkuta nabii huyo akipumzika chini ya mti mkubwa na kumwambia: “Njoo pamoja nami nyumbani, ule mkate.” Mtu wa Mungu wa kweli anapokataa mwaliko huo, mwanamume huyo mzee anasema: “Mimi pia ni nabii kama wewe, na malaika alisema nami kwa neno la Yehova hivi, ‘Mrudishe pamoja nawe nyumbani kwako ili ale mkate na anywe maji.’” Lakini Maandiko yanasema: “Alimdanganya.”—1 Fal. 13:11-18.
9. Maandiko yanasema nini kuhusu wadanganyifu, nao wanawadhuru nani?
9 Hata ingawa hatujui nia ya nabii huyo mzee, ukweli ni kwamba alidanganya. Labda wakati fulani mwanamume huyo mzee alikuwa nabii mwaminifu wa Yehova. Hata hivyo, wakati huu, alikuwa akidanganya. Maandiko yanashutumu vikali mwenendo kama huo. (Soma Methali 3:32.) Wadanganyifu wanaharibu hali yao wenyewe ya kiroho na mara nyingi wanawadhuru wengine kiroho.
“Akarudi Pamoja” na Yule Mwanamume Mzee
10. Nabii wa Mungu alitenda jinsi gani alipoalikwa na mwanamume mzee, na matokeo yalikuwa nini?
10 Nabii huyo kutoka Yuda alipaswa kutambua ujanja wa nabii huyo mzee. Alipaswa kujiuliza, ‘Kwa nini Yehova anamtuma malaika kwa mtu mwingine akiwa na maagizo tofauti kwa ajili yangu?’ Nabii huyo angemwomba Yehova afafanue mwongozo huo waziwazi, lakini Maandiko hayaonyeshi kwamba alifanya hivyo. Badala yake, ‘alirudi pamoja na yule mwanamume mzee ili ale mkate nyumbani kwake na kunywa maji.’ Yehova hakufurahi. Mwishowe, nabii aliyedanganywa alipokuwa njiani akirudi Yuda, alikutana na simba na simba huyo akamuua. Huo ulikuwa mwisho wenye kusikitisha kama nini kwa kazi yake akiwa nabii!—1 Fal. 13:19-25.a
11. Ahiya aliweka mfano gani mzuri?
11 Kwa upande mwingine, nabii Ahiya, aliyetumwa kumtia mafuta Yeroboamu ili awe mfalme, alibaki mwaminifu hata alipokuwa mzee. Ahiya alipozeeka na kuwa kipofu, Yeroboamu alimtuma mke wake amuulize Ahiya kuhusu hali ya mwana wao aliyekuwa mgonjwa. Kwa ujasiri, Ahiya alitabiri kwamba mwana wa Yeroboamu angekufa. (1 Fal. 14:1-18) Ahiya alipata baraka nyingi kutia ndani pendeleo la kuchangia habari iliyotumiwa kuandika Neno la Mungu lililoongozwa na roho. Jinsi gani? Baadaye, kuhani Ezra alitumia maandishi ya Ahiya kuwa chanzo cha habari yake.—2 Nya. 9:29.
12-14. (a) Tunaweza kujifunza somo gani kutokana na yale yaliyompata yule nabii kijana? (b) Toa mifano inayoonyesha uhitaji wa kusali na kufikiria kwa uzito mashauri yanayotegemea Biblia ambayo yanatolewa na wazee.
12 Biblia haisemi kwa nini nabii huyo kijana hakumuuliza Yehova kabla ya kurudi kula na kunywa pamoja na nabii yule mzee. Je, inawezekana kwamba yule mwanamume mzee alimweleza nabii huyo mambo ambayo alitaka kusikia? Tunapata somo gani hapa? Tunapaswa kusadiki kabisa kwamba matakwa ya Yehova ni ya uadilifu. Na tunapaswa kuazimia kuyafuata kwa vyovyote vile.
-
-
Dumisha Ushikamanifu Ukiwa na Moyo KamiliMnara wa Mlinzi—2008 | Agosti 15
-
-
Uwe Mwenye Kiasi
15. Tunajifunza nini kutokana na kosa la nabii wa Mungu?
15 Tunaweza kujifunza jambo gani lingine kutokana na kosa lililofanywa na yule nabii kutoka Yuda? Andiko la Methali 3:5 linasema hivi: “Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe.” Badala ya kuendelea kumtegemea Yehova kama alivyofanya wakati uliopita, mara hii nabii huyo kutoka Yuda alitegemea akili zake mwenyewe. Kwa sababu ya kosa hilo, alipoteza uhai wake na uhusiano wake mzuri pamoja na Mungu. Mambo yaliyompata yanakazia vizuri sana umuhimu wa kuwa wenye kiasi na washikamanifu tunapomtumikia Yehova!
-