-
Kwa Nini Ujiweke Wakfu kwa Yehova?Mnara wa Mlinzi—2010 | Januari 15
-
-
Faida za Kujiweka Wakfu
4. Urafiki kati ya Daudi na Yonathani unatuonyesha nini kuhusu kuwajibika?
4 Wakfu wa Kikristo ni jambo zito. Ni zaidi ya kutimiza wajibu tu. Hata hivyo, tunapata faida gani tunapojiweka wakfu? Kwa mfano, hebu tuone faida za kuwajibika katika mahusiano ya kibinadamu, kama vile uhusiano kati ya marafiki. Ili ufurahie pendeleo la kuwa na rafiki, ni lazima ukubali daraka la kuwa rafiki. Hilo linahusisha kujitoa kabisa, yaani, kuhisi kwamba una daraka au wajibu wa kumjali rafiki yako. Urafiki kati ya Daudi na Yonathani ni kati ya urafiki wa pekee sana katika Biblia. Hata walifanya agano la urafiki kati yao. (Soma 1 Samweli 17:57; 18:1, 3.) Ingawa si rahisi kupata marafiki wanaojitoa kufikia hatua hiyo, mara nyingi urafiki unasitawi wakati watu wanapojitoa kabisa, au kuhisi kwamba wana wajibu au daraka kuelekea marafiki wao.—Met. 17:17; 18:24.
5. Mtumwa angefanya nini ili aendelee kuwa mali ya bwana mzuri?
5 Sheria ambayo Mungu aliwapa Waisraeli inaeleza kuhusu uhusiano mwingine ambao uliwanufaisha watu walipojitoa kabisa. Ikiwa mtumwa alitaka kuendelea kuwa mali ya bwana wake mzuri, angeweza kufanya makubaliano ya kudumu yenye masharti pamoja na bwana huyo. Sheria hiyo inasema hivi: “Ikiwa mtumwa huyo atasisitiza kusema, ‘Nampenda bwana wangu kwelikweli, mke wangu na wanangu; sitaki kuondoka kama mtu aliyewekwa huru,’ basi bwana wake atamleta karibu na Mungu wa kweli naye atamleta kwenye mlango au kwenye mwimo wa mlango; naye bwana wake atalichoma sikio lake na kulitoboa kwa sindano, naye atakuwa mtumwa wake mpaka wakati usio na kipimo.”—Kut. 21:5, 6.
6, 7. (a) Watu wanapata faida gani wanapowajibika? (b) Hilo linaonyesha nini kuhusu uhusiano wetu pamoja na Yehova?
6 Ndoa ni uhusiano ambao unahitaji watu wajitoe kabisa au kuwajibika kwa kadiri kubwa sana. Mtu anawajibika kwa mtu mwingine bali si kwa mkataba au makubaliano. Mwanamume na mwanamke ambao wanaishi pamoja bila kufunga ndoa hawawezi kamwe kuwa na usalama wa kweli; wala watoto wao hawawezi kuwa salama. Lakini wenzi wa ndoa ambao wamejitoa kabisa kwa mmoja na mwenzake katika ndoa inayoheshimika wana sababu ya Kimaandiko inayowachochea wajitahidi kusuluhisha matatizo kwa njia ya upendo.—Mt. 19:5, 6; 1 Kor. 13:7, 8; Ebr. 13:4.
7 Katika nyakati za Biblia, watu walifaidika kwa kufanya makubaliano yenye masharti katika biashara na katika kazi. (Mt. 20:1, 2, 8) Ndivyo ilivyo leo. Kwa mfano, tunafaidika tunapoandika mkataba au makubaliano yenye masharti, kabla ya kuanza biashara au kufanya kazi katika kampuni fulani. Hivyo, ikiwa kujitoa au kuwajibika kunaboresha mahusiano kati ya marafiki, wenzi wa ndoa, na wafanyakazi wenzako, bila shaka utapata faida hata zaidi ukijiweka wakfu bila masharti katika uhusiano wako pamoja na Yehova! Acheni sasa tuone jinsi ambavyo watu walifaidika kwa kujiweka wakfu kwa Yehova Mungu wakati uliopita na jinsi walivyofanya mengi zaidi kuliko tu kujitoa kwake.
Jinsi Waisraeli Walivyofaidika kwa Kujiweka Wakfu kwa Mungu
8. Kujiweka wakfu kwa Mungu kulimaanisha nini kwa Waisraeli?
8 Kwa ujumla, taifa la Israeli lilijiweka wakfu kwa Yehova lilipoweka nadhiri kwa Mungu. Yehova aliwaagiza wakusanyike karibu na Mlima Sinai, kisha akawaambia hivi: “Ikiwa mtaitii sauti yangu kabisa na kulishika kwa kweli agano langu, ndipo hakika mtakapokuwa mali yangu ya pekee kutoka kati ya vikundi vingine vyote vya watu.” Watu wote wakajibu hivi kwa pamoja: “Yote ambayo Yehova amesema tuko tayari kuyafanya.” (Kut. 19:4-8) Waisraeli walipojiweka wakfu, walihitaji kufanya mengi zaidi ya kujitoa tu kufanya jambo fulani. Ilimaanisha kwamba walikuwa mali ya Yehova, na Yehova aliwatendea kama ‘mali yake ya pekee.’
9. Waisraeli walifaidika jinsi gani kwa sababu ya kujiweka wakfu kwa Mungu?
9 Waisraeli walifaidika kwa sababu ya kuwa mali ya Yehova. Yehova alikuwa mshikamanifu naye aliwatunza kama vile mzazi mwenye upendo anavyomtunza mtoto wake. Mungu aliwaambia hivi Waisraeli: “Je, mke anaweza kumsahau mtoto wake anayenyonya hivi kwamba asimhurumie mwana wa tumbo lake? Hata hawa wanawake wanaweza kusahau, lakini mimi mwenyewe sitakusahau wewe.” (Isa. 49:15) Yehova aliwapa Sheria ili iwaongoze, aliwatia moyo kupitia manabii, na akawalinda kwa kutumia malaika. Mtunga-zaburi mmoja aliandika hivi: “Anamtangazia Yakobo neno lake, na Israeli masharti yake na maamuzi yake ya hukumu. Hajafanya hivyo kwa taifa lingine lolote.” (Zab. 147:19, 20; soma Zaburi 34:7, 19; 48:14.) Kama Yehova alivyolitunza taifa ambalo lilikuwa mali yake zamani, ndivyo atakavyowatunza wale wanaojiweka wakfu kwake leo.
-
-
Kwa Nini Ujiweke Wakfu kwa Yehova?Mnara wa Mlinzi—2010 | Januari 15
-
-
Kujiweka Wakfu kwa Mungu Kunaleta Furaha
16, 17. Kwa nini kujiweka wakfu kwa Yehova kunaleta furaha?
16 Kujiweka wakfu kwa Yehova kunaleta furaha kwa sababu kunahusisha kujitoa wenyewe. Yesu alisema ukweli huu wa msingi: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Mdo. 20:35) Yesu alipata furaha kamili ya kutoa wakati wa huduma yake hapa duniani. Nyakati nyingine alikosa wakati wa kupumzika, kula, na kujifurahisha ili awasaidie wengine kupata barabara ya uzima. (Yoh. 4:34) Yesu alifurahia kuufanya moyo wa Baba yake ushangilie. Yesu alisema hivi: “Sikuzote mimi hufanya mambo yanayompendeza.”—Yoh. 8:29; Met. 27:11.
17 Hivyo, Yesu aliwaonyesha wafuasi wake jinsi ya kuwa na maisha yenye kuridhisha aliposema: “Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe.” (Mt. 16:24) Tunapofanya hivyo tunamkaribia Yehova zaidi. Je, kuna mtu mwingine yeyote ambaye anaweza kututunza kwa upendo mwingi hivyo tukijiweka mikononi mwake?
18. Kwa nini kuishi kupatana na wakfu wetu kwa Yehova kunaleta furaha zaidi kuliko kujiweka wakfu kwa kitu chochote au mtu mwingine yeyote?
18 Kujiweka wakfu kwa Yehova na kuishi kupatana na wakfu huo kwa kufanya mapenzi yake kunaleta furaha zaidi kuliko kujiweka wakfu kwa kitu chochote au mtu mwingine yeyote. Kwa mfano, watu wengi wanatumia maisha yao yote kutafuta utajiri lakini hawatosheki wala kupata furaha ya kweli. Hata hivyo, wale wanaojiweka wakfu kwa Yehova wanapata furaha ya kudumu. (Mt. 6:24) Wanafurahi kwa sababu wana pendeleo la kuwa “wafanyakazi wenzi wa Mungu,” hata hivyo, hawajajiweka wakfu kwa kazi fulani bali wamejiweka wakfu kwa Mungu wetu mwenye uthamini. (1 Kor. 3:9) Hakuna mtu mwingine anayeweza kuthamini kujidhabihu kwao kuliko Mungu anavyothamini. Hata atawafanya washikamanifu wake wawe vijana tena ili wafaidike na utunzaji wake milele.—Ayu. 33:25; soma Waebrania 6:10.
19. Wale ambao wamejiweka wakfu kwa Yehova wanafurahia pendeleo gani?
19 Unapoweka wakfu maisha yako kwa Yehova unakuwa na uhusiano wa karibu pamoja naye. Biblia inasema hivi: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yak. 4:8; Zab. 25:14)
-