-
Kwa Nini Uwakabidhi Wengine Kazi—Unaweza Kufanya Hivyo Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
-
-
Kwa Nini Uwakabidhi Wengine Kazi—Unaweza Kufanya Hivyo Jinsi Gani?
YEHOVA alianza kuwakabidhi wengine madaraka au kazi muda mrefu kabla ya Dunia kuumbwa. Alimuumba Mwana wake mzaliwa-pekee kisha akaumba ulimwengu wote akimtumia Mwana huyo akiwa “stadi wa kazi.” (Met. 8:22, 23, 30; Yoh. 1:3) Mungu alipowaumba wenzi wawili wa kwanza, aliwaambia ‘wajaze dunia na kuitiisha.’ (Mwa. 1:28) Muumba aliwapa wanadamu kazi ya kupanua Paradiso ya Edeni mpaka ijaze dunia yote. Ndiyo, tangu mwanzo, tengenezo la Yehova limekuwa likiwakabidhi wengine kazi.
-
-
Kwa Nini Uwakabidhi Wengine Kazi—Unaweza Kufanya Hivyo Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
-
-
Kwa Nini Uwakabidhi Wengine Kazi?
Fikiria jinsi Yehova alivyomuumba Mwana wake mzaliwa-pekee na kushiriki naye katika kazi iliyobaki ya uumbaji. Ndiyo, “kwa njia yake vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani, vitu vinavyoonekana na vitu visivyoonekana.” (Kol. 1:16) Muumba angefanya kazi yote peke yake, lakini alitaka Mwana wake apate pia shangwe iliyotokana na kutimiza kazi hiyo nzuri. (Met. 8:31) Hilo lilimsaidia Mwana wake kujifunza mengi zaidi kuhusu sifa za Mungu. Kwa njia fulani, Baba alitumia nafasi hiyo kumzoeza Mwana wake mzaliwa-pekee.
-