-
‘Yesu Aliwapenda Mpaka Mwisho’‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
16, 17. Yesu aliwapa wanafunzi wake kazi gani?
16 Yesu alionyesha kwamba anawatumaini wanafunzi wake kwa kuwapa kazi mbalimbali. Pindi mbili alipotokeza chakula kingi kimuujiza na kulisha umati wa watu, aliwapa wanafunzi wake kazi ya kugawa chakula hicho. (Mathayo 14:19; 15:36) Aliwapa Petro na Yohana mgawo wa kwenda Yerusalemu na kufanya matayarisho kwa ajili ya Pasaka yake ya mwisho. Walitafuta mwana-kondoo, divai, mkate usio na chachu, mboga chungu za majani, na vitu vingine vya maana vilivyohitajiwa. Huo haukuwa mgawo mdogo, kwa kuwa Sheria ya Musa iliagiza Pasaka iadhimishwe ifaavyo, naye Yesu alihitaji kutii Sheria hiyo. Isitoshe, baadaye usiku huo, Yesu alitumia divai hiyo na mkate huo usio na chachu kuwa mifano muhimu alipoanzisha Ukumbusho wa kifo chake.—Mathayo 26:17-19; Luka 22:8, 13.
17 Yesu aliwapa wanafunzi wake madaraka mazito hata zaidi. Kama tulivyoona mapema, alikikabidhi kikundi kidogo cha wafuasi wake watiwa-mafuta hapa duniani daraka zito la kutayarisha na kugawa chakula cha kiroho. (Luka 12:42-44) Pia, kumbuka kwamba aliwapa wanafunzi wake kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (Mathayo 28:18-20) Hata sasa, ingawa anatawala mbinguni na hatuwezi kumwona, Yesu amewapa watu wenye sifa za kiroho, “zawadi katika wanadamu,” daraka la kutunza kutaniko lake lililo duniani.—Waefeso 4:8, 11, 12.
-
-
‘Yesu Aliwapenda Mpaka Mwisho’‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
19 Je, tunaweza kumwiga Yesu kwa kuwa tayari kuwapa wengine mapendeleo? Ndugu walio na madaraka kutanikoni wanapaswa kuwapa wengine migawo inayowafaa na inayotimiza kusudi fulani wakiamini kwamba ndugu hao watafanya yote wanayoweza. Kwa njia hiyo, wazee wenye uzoefu wanaweza kuwazoeza vijana wanaostahili ambao ‘wanajitahidi kufikia’ mapendeleo ya kulisaidia kutaniko. (1 Timotheo 3:1; 2 Timotheo 2:2) Mazoezi hayo ni ya maana. Yehova anapoendelea kuharakisha ukuzi wa Ufalme, wanaume wanaostahili watahitaji kuzoezwa kushughulikia ongezeko hilo.—Isaya 60:22.
-