-
Siri Takatifu ya Mungu—Upeo Wayo Wenye Utukufu!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
5. Katika 1928, ni nini kilichotukia kwenye mkusanyiko wa Wanafunzi wa Biblia ambacho kilikazia tarumbeta ya saba?
5 Ule mpigo wa tarumbeta ya malaika wa saba ulirudishwa katika mambo makuu ya mkusanyiko wa Wanafunzi wa Biblia katika Detroit, Michigan, Julai 30–Agosti 6, 1928. Wakati huo stesheni za usambazaji 107 zilifunganishwa katika kile ambacho The New York Times lilikielezea kuwa ‘mfunganisho wa redio wenye kuenea na kugharimu zaidi sana katika historia.’ Mkusanyiko huo ulikubali kwa idili “Julisho-wazi [lenye nguvu sana] Dhidi ya Shetani na kwa Ajili ya Yehova,” likielekeza kwenye upinduzi wa Shetani na tengenezo lake mbovu kwenye Har–Magedoni, na kuwekwa huru kwa wote wanaopenda uadilifu. Raia washikamanifu wa Ufalme wa Mungu walipendezwa sana kupokea kitoleo cha mkusanyiko, kile kitabu cha kurasa 368 Government. Hicho kilitoa ithibati zilizo wazi zaidi “kwamba Mungu aliweka Mfalme Mpakwa-Mafuta wake juu ya kiti cha ufalme katika 1914.”
-
-
Siri Takatifu ya Mungu—Upeo Wayo Wenye Utukufu!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
7. 1928 Detroit, Michigan: Julisho-wazi dhidi ya Shetani na kwa ajili ya Yehova, likionyesha wazi kwamba Mfalme mpakwa-mafuta wa Mungu, aliyeketishwa katika kiti cha ufalme 1914, ataharibu tengenezo bovu la Shetani na kuweka huru aina ya binadamu.
-