Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mfikirieni Sana Yeye Ambaye Amevumilia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • 12 Lazima Yesu alijaribiwa pia na udhaifu wa wanafunzi wake wa karibu. Kama tulivyojifunza katika Sura ya 3, walionyesha tena na tena tamaa ya kujitakia makuu. (Mathayo 20:20-24; Luka 9:46) Zaidi ya mara moja, Yesu aliwashauri kwamba wanahitaji kuwa wanyenyekevu. (Mathayo 18:1-6; 20:25-28) Hata hivyo iliwachukua muda mrefu kusitawisha sifa hiyo. Wazia kwamba hata usiku wa mwisho aliokuwa pamoja nao, bado walikuwa na “bishano kali” kuhusu ni nani kati yao aliye mkuu zaidi ya wote! (Luka 22:24) Je, Yesu aliona kwamba hawawezi kubadilika, naye akaacha kujaribu kuwasaidia? Hapana. Akiwa mwenye subira kama kawaida yake, aliendelea kuwa na tumaini na maoni yanayofaa, akiendelea kuona sifa nzuri walizokuwa nazo. Alijua kwamba walimpenda Yehova kutoka moyoni na kwa kweli walitaka kufanya mapenzi Yake.—Luka 22:25-27.

      Picha katika ukurasa wa 70

      Tutaruhusu upinzani upunguze bidii yetu, au tutaendelea kuhubiri kwa bidii?

      13. Kama Yesu, huenda tukakabili majaribu gani?

      13 Tunaweza kupatwa na majaribu kama yale ambayo Yesu alivumilia.

  • “Mfikirieni Sana Yeye Ambaye Amevumilia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • Picha katika ukurasa wa 70

      Tutaruhusu upinzani upunguze bidii yetu, au tutaendelea kuhubiri kwa bidii?

      Hali ya kutokamilika ya ndugu zetu Wakristo inaweza kujaribu imani yetu. Wanaweza kusema au kutenda bila kufikiri na hivyo kuumiza hisia zetu. (Methali 12:18) Je, tutaacha udhaifu wa waamini wenzetu utufanye tuone kwamba hawafai, au tutaendelea kuvumilia udhaifu wao na kukazia fikira sifa zao nzuri?—Wakolosai 3:13.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki