Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuelewa Kusudi la Nidhamu
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 1
    • Nidhamu ya Wazazi Wenye Upendo

      Katika familia na katika kutaniko la Kikristo, wote wanahitaji kuelewa kusudi la nidhamu, hasa wale wenye madaraka, kama vile wazazi. Andiko la Mithali 13:24, NW, linasema: “Anayezuia fimbo yake anamchukia mwana wake, lakini anayempenda ni yule anayemwangalia kwa nidhamu.”

      Wazazi wanapaswa kutoa nidhamu kwa njia gani? Biblia inasema: “Nanyi, akina baba, msiwe mkiwasumbua watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika nidhamu na rekebisho la akilini la Yehova.” (Waefeso 6:4) Shauri hilo linarudiwa katika maneno haya: “Nyinyi akina baba, msiwe mkichochea watoto wenu wakasirike, ili wasishuke moyo.”—Wakolosai 3:21.

      Wazazi Wakristo wanaoelewa kusudi la nidhamu hawatakuwa wakali. Kanuni inayotajwa katika 2 Timotheo 2:24 inaweza kutumiwa kuhusiana na jinsi wazazi wanavyotoa nidhamu. Paulo aliandika: “Mtumwa wa Bwana hahitaji kupigana, bali ahitaji kuwa mwanana kuelekea wote, mwenye sifa za ustahili kufundisha.” Bila shaka, hasira nyingi isiyozuiwa, kusema kwa sauti kubwa, na matusi au maneno yenye kutia aibu si nidhamu ya upendo, nao Wakristo hawapaswi kuyatumia kamwe.—Waefeso 4:31; Wakolosai 3:8.

      Rekebisho la wazazi linahusisha mengi zaidi ya adhabu inayotolewa haraka-haraka pasipo kusita. Watoto wengi wanahitaji kushauriwa mara kadhaa kabla ya kurekebisha maoni yao. Hivyo, wazazi wanapaswa kutumia wakati, kuwa wenye subira, na kufikiria kwa makini jinsi wanavyotoa nidhamu. Ni lazima wakumbuke kwamba watoto wanapaswa kulelewa katika “nidhamu na rekebisho la akilini la Yehova.” Mafundisho hayo huendelea kwa miaka mingi.

  • Kuelewa Kusudi la Nidhamu
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 1
    • Yehova Ndiye Hakimu Mkamilifu

      Wazazi, wachungaji Wakristo, na wengine walio na mamlaka ya Kimaandiko ya kutoa nidhamu wanapaswa kuchukua daraka hilo kwa uzito. Hawapaswi kukata kauli kimbele kwamba wengine hawawezi kurekebika. Kwa hiyo, nidhamu wanayotoa haipaswi kamwe kuwa adhabu kali au ya kulipiza kisasi.

      Naam, Biblia humtaja Yehova kuwa ndiye atakayetoa adhabu kali na ya mwisho. Kwa kweli, Biblia husema kwamba “ni jambo lenye kuhofisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai.” (Waebrania 10:31) Lakini hakuna mwanadamu yeyote anayepaswa kujaribu kujilinganisha na Yehova kwa kutoa adhabu kali au katika njia nyingine yoyote. Na hakuna mtu yeyote anayepaswa kuhisi kwamba ni jambo lenye kuhofisha kuanguka katika mikono ya mzazi au mzee fulani kutanikoni.

      Yehova ana uwezo wa kuonyesha usawaziko kwa njia kamilifu anapotoa nidhamu. Wanadamu hawawezi. Mungu anaweza kusoma mioyo na kutambua wakati mtu amefikia hatua ya kutoweza kurekebishwa na hivyo kustahili kupata adhabu ya mwisho kabisa. Kwa upande mwingine, wanadamu hawana uwezo wa kutoa hukumu kama hiyo. Kwa sababu hiyo, inapokuwa lazima kutoa nidhamu, sikuzote wale walio na mamlaka wanapaswa kufanya hivyo wakiwa na kusudi la kumrekebisha mkosaji.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki