-
Shikamana na Tengenezo la YehovaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
kuwa waangalizi. (Ebr. 13:7, 17) Tukifuata kwa ukaribu mipango ya kitheokrasi na kushirikiana na wale wanaoongoza, tutakuwa tayari kufanya mapenzi ya Yehova. Tunahitaji kutumia kikamili pendeleo la sala. Kumbuka kwamba kuta za gereza wala kifungo cha upweke hakiwezi kutuzuia kuwasiliana na Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo wala kuvuruga umoja uliopo kati yetu na waamini wenzetu.
21 Kwa uvumilivu, na tuazimie kufanya yote tunayoweza ili kutimiza utume wetu wa kuhubiri, tukidumu katika kazi ambayo Yesu Kristo aliyefufuliwa aliwaagiza wafuasi wake wafanye: “Basi, nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, mkiwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, na kuwafundisha kushika mambo yote niliyowaamuru. Na tazama! mimi nipo pamoja nanyi sikuzote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mt. 28:19, 20) Kama Yesu, natuvumilie. Acheni tukazie macho tumaini la Ufalme na tarajio la uzima wa milele lililo mbele yetu. (Ebr. 12:2) Tukiwa wanafunzi waliobatizwa wa Kristo, tuna pendeleo la kushiriki kutimiza unabii wa Yesu kuhusu “umalizio wa mfumo wa mambo.” Alisema hivi: “Habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mt. 24:3, 14) Tukifanya kazi hiyo kwa moyo wetu wote wakati huu, tutafurahia uzima wa milele katika ulimwengu mpya wa Yehova wenye uadilifu!
-
-
NyongezaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
Nyongeza
Ujumbe kwa Wazazi Wakristo:
Ukiwa mzazi, ungependa kuwasaidia watoto wako wapendwa wampende Yehova na kujiweka wakfu kwake. Unaweza kufanya nini ili uwasaidie wajitayarishe kwa ajili ya ubatizo? Utajuaje kwamba wako tayari kwa ajili ya hatua hiyo muhimu?
Yesu aliwaagiza wanafunzi wake hivi: ‘Fanyeni wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, na kuwabatiza.’ (Mt. 28:19) Kulingana na agizo hilo, takwa la msingi ili mtu astahili kubatizwa ni kuwa mwanafunzi, yaani, anapaswa kuelewa, kuamini, na kujitahidi kuishi kupatana na mafundisho ya Yesu. Hata watoto wanaweza kutimiza jambo hilo.
Wawekee watoto wako kielelezo chema, na ukazie sheria za Yehova mioyoni mwao. (Kum. 6:6-9) Unaweza kutumia habari zilizo katika kitabu Furahia Maisha Milele! ili kuwafundisha kweli za msingi na jinsi ya kuishi kulingana na kanuni za Biblia. Wasaidie watoto wako wajue jinsi ya kueleza mambo wanayoamini kwa maneno yao wenyewe wanapoongea na wengine. (1 Pet. 3:15) Kitia-moyo na ujuzi wanaopokea kutoka kwako pamoja na mambo wanayojifunza kibinafsi, ibada ya familia, mikutano ya kutaniko, na marafiki wazuri, yatawasaidia kufikia ubatizo na kufanya maendeleo zaidi. Wasaidie wajiwekee miradi ya kiroho.
-