-
Upendo Hushinda ChukiAmkeni!—2009 | Agosti
-
-
Upendo Hushinda Chuki
“Jamii mpya ya kidini ilitokea kwa mara ya kwanza katika historia: si kikundi fulani kinachoendeleza utaifa, lakini kikundi cha wajitoleaji ambao wameshinda tofauti za kijamii, rangi, na kitaifa: wanaume kwa wanawake wakiungana kwa usawa mbele ya mungu wao.”—Kitabu cha Paul Johnson, A History of Christianity.
UKRISTO wa kweli ulipoenea kotekote katika Milki ya Roma, watu waliona jambo la kushangaza—familia ya kimataifa ya watu wanaomwabudu Mungu ambao wamejifunza kuishi pamoja kwa amani ya kweli na umoja. Siri ya “familia” hiyo kuwa na amani ilikuwa upendo wa kweli uliotegemea kanuni za Mungu wala si hisia tu.
-
-
Upendo Hushinda ChukiAmkeni!—2009 | Agosti
-
-
Mungu Ni Mwenye Subira Kwetu
Katika karne ya kwanza, Wakristo wengi Wayahudi waliathiriwa na maoni yenye ubaguzi kuelekea watu wasio Wayahudi, ambao wengi wao waligeuka na kuwa waamini. Yehova Mungu alishughulikiaje jambo hilo ambalo lingeweza kuwagawanya watu? Alilifundisha kutaniko la Kikristo kwa subira. (Matendo 15:1-5) Subira hiyo ilikuwa na matokeo mazuri, kwa kuwa kama ilivyotajwa mwanzoni mwa makala hii, ‘walishinda tofauti za kijamii, rangi, na kitaifa.’ Kwa sababu hiyo, “makutaniko yakaendelea kufanywa imara katika imani na kuongezeka hesabu siku baada ya siku.”—Matendo 16:5.
-