-
Upendo Hushinda ChukiAmkeni!—2009 | Agosti
-
-
Lakini, Mungu anamwonaje mtu mwenye ubaguzi anayejitahidi kuondoa hisia hizo moyoni mwake? Biblia inasema mambo yenye kufariji kuhusu jambo hilo.
Mungu Ni Mwenye Subira Kwetu
Katika karne ya kwanza, Wakristo wengi Wayahudi waliathiriwa na maoni yenye ubaguzi kuelekea watu wasio Wayahudi, ambao wengi wao waligeuka na kuwa waamini. Yehova Mungu alishughulikiaje jambo hilo ambalo lingeweza kuwagawanya watu? Alilifundisha kutaniko la Kikristo kwa subira. (Matendo 15:1-5) Subira hiyo ilikuwa na matokeo mazuri, kwa kuwa kama ilivyotajwa mwanzoni mwa makala hii, ‘walishinda tofauti za kijamii, rangi, na kitaifa.’ Kwa sababu hiyo, “makutaniko yakaendelea kufanywa imara katika imani na kuongezeka hesabu siku baada ya siku.”—Matendo 16:5.
Tunajifunza nini? Usikate tamaa, lakini endelea kumwomba Mungu msaada kwa kuwa yeye anawapa hekima na nguvu za kufanya yaliyo sawa wale ‘wanaoendelea kuomba kwa imani.’ (Yakobo 1:5, 6) Je, unawakumbuka Jennifer, Timothy, John, na Olga waliotajwa katika makala ya kwanza ya mfululizo huu? Jennifer alipoenda kwenye shule ya sekondari, alikuwa amekomaa kiroho na alikuwa amejifunza kupuuza matusi kuhusu rangi na kimo chake. Muda mfupi baadaye, msichana mwingine alipotukanwa mara nyingi na wanafunzi wenzake, Jennifer alimtetea na kumfariji.
Ni nini kilichomsaidia Timothy kuwa mtulivu wanafunzi wenzake walipomtukana kwa sababu ya rangi yake? Anasema: “Sikutaka kuliletea suto jina la Yehova Mungu. Pia nilikumbuka kwamba tunapaswa ‘kuendelea kuushinda uovu kwa wema’ na kutoruhusu uovu utushinde.”—Waroma 12:21.
John alishinda hisia zake za ubaguzi dhidi ya mwanafunzi mwenzake ambaye ni Mhausa. “Nilipokuwa kijana,” anasema, “nilikutana na wanafunzi Wahausa na tukawa marafiki. Nilifanya mradi mmoja wa shule pamoja na mmoja wao, na tulipatana sana. Sasa ninajitahidi kuwaona watu jinsi walivyo, si kwa kutegemea rangi au kabila lao.”
Olga na mmishonari mwenzake hawakuogopa walipoteswa na wapinzani wenye chuki, lakini waliendelea kuwa imara, wakiwa na uhakika kwamba watu fulani watathamini ujumbe wa Biblia. Wengi waliuthamini. “Miaka 50 hivi baadaye,” anasema Olga, “mwanamume mmoja alinipa mfuko maridadi sana. Ndani yake kulikuwa na mawe madogo yaliyokuwa yameandikwa sifa za Kikristo kama vile wema, fadhili, upendo, na amani. Kisha aliniambia kwamba alikuwa mmoja wa wale wavulana walionitupia mawe na sasa yeye ni ndugu yangu Mkristo. Yeye na mke wake wakanipa maua meupe 24 ya waridi pamoja na ule mfuko wenye mawe.”
-
-
Upendo Hushinda ChukiAmkeni!—2009 | Agosti
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa8, 9]
KANUNI ZA MUNGU TUNAZOPASWA KUFUATA
◼ “Msimlipe yeyote uovu kwa uovu. . . . Endelea kuushinda uovu kwa wema.” (Waroma 12:17-21) Tunajifunza nini? Wengine wakikutendea mambo mabaya, jifunze kuwatendea kwa njia nzuri. “Walinichukia bila sababu,” alisema Yesu Kristo. Hata hivyo, yeye hakuwachukia.—Yohana 15:25.
◼ “Na tusiwe wenye kujisifu, . . . tukioneana wivu.” (Wagalatia 5:26) Wivu na kiburi hudhuru hali ya kiroho, na mara nyingi humfanya mtu awe na chuki na ubaguzi.—Marko 7:20-23.
◼ “Kwa hiyo, mambo yote mnayotaka watu wawatendee ninyi, lazima mwatendee wao pia vivyo hivyo.” (Mathayo 7:12) Jiulize, ‘Ningependa kutendewa jinsi gani?’ Watendee watu wengine kwa njia hiyo, haidhuru wana umri, rangi, utamaduni au wanazungumza lugha gani.
◼ “Mkaribishane, kama vile Kristo pia alivyotukaribisha sisi.” (Waroma 15:7) Je, wewe hujaribu kuwafahamu watu wa malezi na utamaduni mbalimbali, hasa ikiwa wao ni watumishi wenzako wa Mungu?—2 Wakorintho 6:11.
◼ “Hata ikiwa baba yangu na mama yangu wangeniacha, Yehova mwenyewe angenichukua.” (Zaburi 27:10) Hata wengine wakutendee namna gani, Mungu hatakuacha kamwe ukiendelea kuwa mshikamanifu kwake.
-