-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2006 | Julai 15
-
-
Mwenendo mpotovu (Kigiriki, a·selʹgei·a) unahusisha “ufisadi; ufasiki; mwenendo wa kukosa aibu; mwenendo wa ukware.” Kamusi moja (The New Thayer’s Greek-English Lexicon) inafafanua neno hilo la Kigiriki kuwa “uchu usiozuilika, . . . kupita kiasi, kutokuwa na aibu, ufidhuli.” Kulingana na kamusi nyingine, mwenendo mpotovu ni tabia “inayokiuka mipaka yote ya mambo yanayokubalika katika jamii.”
Kama vile maelezo hayo yanavyoonyesha, “mwenendo mpotovu” unatia ndani mambo mawili: (1) Mwenendo wenyewe unakiuka kabisa sheria za Mungu, na (2) mtazamo wa mkosaji ni wa kukosa heshima na wa ufidhuli.
Hivyo, “mwenendo mpotovu” haurejelei mwenendo mbaya katika mambo madogo. Unahusiana na matendo ambayo yanavunja kabisa sheria za Mungu na ambayo yanaonyesha mtazamo wa kikaidi au wa dharau, yaani, mtazamo ambao unaonyesha ukosefu wa heshima au hata dharau kuelekea mamlaka, sheria, na kanuni za maadili. Paulo anahusianisha mwenendo mpotovu na ngono haramu. (Waroma 13:13, 14) Kwa kuwa andiko la Wagalatia 5:19-21 linaorodhesha mwenendo mpotovu kati ya mazoea yenye dhambi ambayo yanaweza kumfanya mtu asistahili kuurithi Ufalme wa Mungu, ni wazi kwamba mtu anaweza kukaripiwa au hata kutengwa na ushirika wa kutaniko la Kikristo kwa sababu ya kuhusika katika mwenendo mpotovu.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2006 | Julai 15
-
-
Sikuzote, maneno ya Kimaandiko “mwenendo mpotovu” yanahusisha dhambi nzito, kwa kawaida dhambi ya kingono. Wazee wanapojaribu kutambua mwenendo mpotovu, wanapaswa kuangalia waone ikiwa dhambi hiyo inahusisha ukaidi, ufasiki, uchafu, kutokuwa na aibu, na ikiwa ni jambo linalowashangaza watu kwa jumla.
-