Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Novemba 1
    • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

      Kutaniko la Kikristo huonaje ulafi?

      Neno la Mungu hushutumu ulevi na ulafi kuwa tabia zisizowafaa wale wanaomtumikia Mungu. Kwa hiyo, kutaniko la Kikristo humwona mlafi asiyetaka kubadilika kwa njia ileile linavyomwona mtu aliye na zoea la ulevi. Mlevi au mlafi hawezi kuwa mshiriki wa kutaniko la Kikristo.

      Methali 23:20, 21 inasema: “Usiwe kati ya watu wanaokunywa divai mno, kati ya watu wanaokula nyama kwa ulafi. Kwa maana mlevi na mlafi watakuwa maskini, na kusinzia kutamvika mtu nguo zilizopasuka.” Katika Kumbukumbu la Torati 21:20 tunasoma kuhusu mtu “mkaidi na mwasi,” ambaye kulingana na Sheria ya Musa alistahili kuuawa. Kulingana na mstari huo, mtu huyo mwasi na asiyetubu alikuwa “mlafi na mlevi.” Ni wazi kwamba katika Israeli la kale, ulafi ulionwa kuwa zoea lisilofaa kwa waliotaka kumtumikia Mungu.

      Hata hivyo, mlafi ni mtu wa aina gani, nayo Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo husema nini kuhusu ulafi? Mlafi ni mtu ambaye “sikuzote hula na kunywa kwa pupa.” Hivyo, ulafi ni aina ya pupa, nalo Neno la Mungu hutuambia kwamba “watu wenye pupa” ni kati ya wale ambao hawataurithi Ufalme wa Mungu. (1 Wakorintho 6:9, 10; Wafilipi 3:18, 19; 1 Petro 4:3) Kwa kuongezea, wakati mtume Paulo alipowaonya Wakristo kuhusu kujihusisha katika “matendo ya mwili,” alitaja pia “vipindi vya kulewa, karamu za kupindukia, na mambo kama hayo.” (Wagalatia 5:19-21) Mara nyingi, kula kupita kiasi huambatana na vipindi vya kulewa na karamu za kupindukia. Isitoshe, ulafi pia unatiwa ndani ya “mambo kama hayo” ambayo Paulo alitaja. Kama ilivyo kuhusiana na ‘matendo mengine ya mwili,’ Mkristo anayejulikana sana kuwa mlafi na anayekataa kwa ukaidi kubadili tabia yake yenye pupa, anapaswa kuondolewa katika kutaniko.—1 Wakorintho 5:11, 13.a

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Novemba 1
    • a Ona “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Mei 1, 1986.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki