-
Onyesha Uaminifu wa Kikristo Mtu wa Ukoo Anapotengwa na UshirikaHuduma ya Ufalme—2002 | Agosti
-
-
8 Ikiwa mtoto anayeishi nyumbani ametengwa na ushirika, wazazi Wakristo bado wana daraka la kumlea. Gazeti Mnara wa Mlinzi la Novemba 15, 1988, lilisema hivi katika ukurasa wa 20: “Sawa na vile ambavyo wao wataendelea kumwandalia chakula, nguo, na makao, wao wanahitaji kumwagiza na kumtia nidhamu kupatana na Neno la Mungu. (Mithali 6:20-22; 29:17) Hivyo wazazi wenye upendo wangeweza kupanga kuwa na funzo la Biblia la kimaskani [nyumbani] pamoja naye, hata ikiwa ametengwa na ushirika. Labda atapata manufaa iliyo na usahihisho mkubwa zaidi kutokana na kujifunza kwao pamoja naye akiwa peke yake. Au wangeweza kuamua kwamba yeye anaweza kuendelea kushiriki katika mpango wa funzo la jamaa.”—Ona pia gazeti Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, 2001, ukurasa wa 16-17.
-
-
Onyesha Uaminifu wa Kikristo Mtu wa Ukoo Anapotengwa na UshirikaHuduma ya Ufalme—2002 | Agosti
-
-
11 Kuhusu mtoto, makala hiyohiyo yaendelea kusema: “Nyakati nyingine wazazi Wakristo wamemkubali arudi nyumbani kwa muda fulani mtoto aliyetengwa na ushirika ambaye amekuwa mgonjwa sana kimwili au katika mawazo yake ya moyoni. Lakini katika kila kisa wazazi wanaweza kuzipima hali za mtu huyo waone ziko namna gani. Je! mwana aliyetengwa na ushirika amekuwa akiishi kwa kujitegemea mwenyewe, na je! sasa hawezi kufanya hivyo? Au yeye anataka kurudi nyumbani kwa sababu hasa akirudi maisha yatakuwa mepesi zaidi? Nazo tabia zake na nia yake iko namna gani? Je! ataingiza ‘chachu’ nyumbani?—Gal. 5:9.”
-