Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi ya Kushughulika na Mtu Aliyetengwa na Ushirika
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
    • Tunaweza kushughulika jinsi gani na mtu wa ukoo aliyetengwa na ushirika? Katika hali kama hiyo, uhusiano wa karibu kati ya watu wa familia unaweza kuwa jaribu kali la ushikamanifu. Tunaweza kushughulika jinsi gani na mtu wa ukoo aliyetengwa na ushirika? Hatuwezi kuzungumzia hali zote zinazoweza kutokea, lakini acheni tuchunguze mbili.

      Katika visa fulani, mtu wa familia aliyetengwa na ushirika huenda bado anaishi katika nyumba moja na wazazi wake na ndugu na dada zake. Kwa kuwa kutengwa na ushirika hakuvunji uhusiano wa kifamilia, shughuli na mambo ya kawaida ya familia yataendelea. Hata hivyo, kupitia mwenendo wake, mtu huyo amechagua kuvunja kifungo cha kiroho kati yake na watu wa familia ambao ni waamini. Kwa hiyo, watu wa familia ambao ni washikamanifu hawataendelea kumshirikisha katika mambo ya kiroho. Kwa mfano, mtu huyo aliyetengwa na ushirika akijiunga na familia wakati inapokutana ili kujifunza Biblia, hatashiriki. Hata hivyo, ikiwa aliyetengwa si mtu mzima, wazazi wake bado wana jukumu la kumfundisha na kumtia nidhamu. Hivyo, wazazi wenye upendo wanaweza kupanga kujifunza naye Biblia.b—Methali 6:20-22; 29:17.

      Katika visa vingine, huenda mtu wa ukoo aliyetengwa na ushirika anaishi kwake mbali na familia yao. Ingawa huenda mara mojamoja kukawa na uhitaji wa kuchangamana naye ili kushughulikia jambo fulani la familia, pindi kama hizo zinapaswa kuwa chache. Watu wa familia ambao ni washikamanifu hawatafuti visingizio vya kuchangamana na mtu aliyetengwa na ushirika ambaye anaishi nje ya familia. Badala yake, ushikamanifu kwa Yehova na tengenezo lake unawachochea kuunga mkono mpango wa Kimaandiko wa kutenga na ushirika. Ushikamanifu wao unaonyesha kwamba wanamjali mkosaji, nao unaweza kumsaidia afaidike kutokana na nidhamu aliyopata.c—Waebrania 12:11.

  • Jinsi ya Kushughulika na Mtu Aliyetengwa na Ushirika
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
    • c Ili upate habari zaidi kuhusu kushughulika na watu wa ukoo ambao wametengwa na ushirika, ona shauri la Kimaandiko lililo katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1988, ukurasa wa 26-31, na la Januari 1, 1982, ukurasa wa 18-24.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki