-
Habari Njema Yazaa Matunda Huko São Tomé na PríncipeMnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 15
-
-
Kusanyiko la Kipekee
Mashahidi wa Yehova katika visiwa vya São Tomé na Príncipe walishuhudia tukio la kipekee wakati Kusanyiko la kwanza la Wilaya la siku tatu lenye kichwa “Ufundishaji wa Kimungu” lilipofanywa Januari 1994 visiwani humo. Lilifanywa katika jumba bora zaidi nchini lenye mfumo wa kusafisha hewa. Je, unaweza kuwazia jinsi watangazaji wa Ufalme 116 walivyofurahi kuona wahudhuriaji 405 na kwa mara ya kwanza wakatazama drama za Biblia na kupokea vichapo vipya kusanyikoni? Watu 20 waliokuwa wamejiweka wakfu walibatizwa kwenye ufuo fulani wa kitropiki.
Watu walivutiwa sana na beji za pekee zilizovaliwa na wajumbe. Wageni 25 waliotoka Ureno na Angola walifanya kusanyiko hilo lionekane kuwa la kimataifa. Uhusiano mchangamfu wa upendo wa Kikristo ulisitawi haraka, na wengi walitokwa na machozi walipoagana baada ya kusanyiko kumalizika.—Yohana 13:35.
Waandishi wa habari kutoka idhaa ya Redio ya Taifa walikuja na kumhoji mwangalizi wa kusanyiko. Pia walitangaza sehemu kadhaa za hotuba zilizotolewa. Hiyo ilikuwa pindi ya pekee kwelikweli, nayo ilisaidia Mashahidi hao waaminifu ambao wameishi mbali kwa muda mrefu wajihisi wako karibu na tengenezo la Yehova linaloonekana.
-
-
Habari Njema Yazaa Matunda Huko São Tomé na PríncipeMnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 15
-
-
2. Lile kusanyiko la wilaya la pekee lilifanywa katika jumba hili
3. Watu wenye furaha wanaotaka kubatizwa kwenye kusanyiko
-