-
Tangazeni Mfalme na Ufalme! (1919-1941)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
“Roho ya Yehova Ilitufanya Tusiwe na Hofu”
Wakati wa 1927, watu wa Yehova walitiwa moyo watumie sehemu ya kila Jumapili katika kutoa ushahidi wa kikundi. Upinzani wa kisheria ukatokezwa mara hiyo. Katika muda wa miaka michache, kukamatwa kukaanza kuongezeka—268 katika Marekani pekee katika 1933, 340 katika 1934, 478 katika 1935, na 1,149 katika 1936. Kwa shtaka gani? Kwa kweli, kwa mashtaka mbalimbali, kutia ndani kuuza bila leseni, kuvuruga amani, na kuhalifu sheria za sabato ya Jumapili.
-
-
Tangazeni Mfalme na Ufalme! (1919-1941)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Hivyo, mapema katika miaka ya 1930, walijipigania kwa kufanya mashambulizi. Jinsi gani? Kwa njia ya kampeni za pekee za kuhubiri zilizojulikana kuwa kampeni za vikundi. Maelfu ya wenye kujitolea kotekote katika Marekani walipangwa kitengenezo katika vikundi. Wakati Mashahidi walipokamatwa katika mji mmoja kwa kuhubiri nyumba hadi nyumba, kikundi cha wenye kujitolea kutoka maeneo mengine kiliwasili upesi na “kushambulia” mji huo, kikitoa ushahidi kamili.e
Kampeni hizo za vikundi zilisaidia sana kuimarisha Mashahidi wenyeji. Katika kila kikundi, mlikuwamo ndugu wenye kustahili ambao walikuwa wamezoezwa kushughulika na wenye mamlaka. Kilikuwa kitia-moyo kikubwa kwa ndugu walioishi katika eneo lenye matata, labda katika mji mdogo, kujua kwamba hawakuwa peke yao katika kupiga mbiu ya Ufalme wa Mungu.
Ilitaka ujasiri mwingi mno kushiriki katika kampeni hizo za vikundi za miaka ya 1930. Katikati ya kipindi cha ule Mshuko Mkubwa wa Kiuchumi, kazi zilikuwa haba. Hata hivyo, Nicholas Kovalak, Jr., mwangalizi asafiriye kwa miaka kama 40, akumbuka hivi: “Mwito ulipokuja wa kueneza eneo lenye matata, ‘mwelekezi wa utumishi’ angeomba wenye kujitolea. Watu mmoja-mmoja waliambiwa wasijitolee ikiwa waliogopa kupoteza kazi zao. . . . Lakini sikuzote tulifurahi kuona itikio thabiti la asilimia 100!” John Dulchinos, mwangalizi mmoja kutoka Springfield, Massachusetts akaonelea: “Kwelikweli, hiyo ilikuwa miaka yenye kusisimua na kumbukumbu zayo ni zenye thamani. Roho ya Yehova ilitufanya tusiwe na hofu.”
-