-
Jinsi ya Kukabiliana na Kuvunjika MoyoMnara wa Mlinzi—2001 | Aprili 15
-
-
● Asafu alilalamika hivi: “Hakika nimejisafisha moyo wangu bure, nimenawa mikono yangu kwa kutokukosa. Maana mchana kutwa nimepigwa, na kuadhibiwa kila asubuhi.”—Zaburi 73:13, 14.
-
-
Jinsi ya Kukabiliana na Kuvunjika MoyoMnara wa Mlinzi—2001 | Aprili 15
-
-
Mkaribie Yehova
Katika Zaburi 73, Asafu aliandika kinaganaga juu ya mfadhaiko wake. Alipolinganisha mafanikio ya waovu na hali yake mwenyewe, aliwaonea wivu. Aliona kwamba wasiomcha Mungu walikuwa wenye kiburi na wajeuri, lakini hawakuadhibiwa. Kisha, Asafu akatilia shaka faida ya kudumisha mwenendo wa haki maishani.—Zaburi 73:3-9, 13, 14.
Kama Asafu, je, umeona jinsi ambavyo waovu wanaojivunia uovu wao huonekana kufanikiwa maishani? Asafu alishindaje hali yake ya kuvunjika moyo? Anasema: “Nami nilifikiri jinsi ya kufahamu hayo; ikawa taabu machoni pangu; hata nilipoingia katika patakatifu pa Mungu, nikautafakari mwisho wao.” (Zaburi 73:16, 17) Asafu alichukua hatua zinazofaa kwa kumwendea Yehova katika sala. Kwa vile mtume Paulo alivyosema, Asafu alizuia “mtu wa kimwili” kwa kuamsha ndani yake mwenyewe “mtu wa kiroho.” Alipopata uelewevu mpya wa kiroho, alifahamu kwamba Yehova huchukia ubaya na katika wakati unaofaa waovu wataadhibiwa.—1 Wakorintho 2:14, 15.
Ni muhimu kama nini kuruhusu Biblia ikusaidie kuona maisha jinsi yalivyo! Yehova anatukumbusha kwamba anaona matendo ya waovu. Biblia yafundisha: “Msiongozwe vibaya: Mungu si wa kudhihakiwa. Kwa maana lolote lile mtu analopanda, hilo atavuna pia . . . Kwa hiyo acheni tusife moyo katika kufanya lililo bora.” (Wagalatia 6:7-9) Yehova atawaweka waovu “penye utelezi”; na kuwaangusha “mpaka palipoharibika.” (Zaburi 73:18) Mwishowe haki ya kimungu itashinda.
Kulishwa kiroho kunakoendelea kwenye meza ya Yehova na ushirika unaofaa pamoja na watu wa Mungu kutaimarisha imani yako na kukusaidia kushinda kuvunjika moyo na hisia nyingine zisizofaa. (Waebrania 10:25) Kama Asafu, ukikaa karibu na Mungu, utaweza kupata msaada wake wenye upendo. Asafu anaongeza: “Mimi ni pamoja nawe daima, umenishika mkono wa kuume. Utaniongoza kwa shauri lako, na baadaye utanikaribisha kwa utukufu.” (Zaburi 73:23, 24) Mkristo mmoja ambaye alitendwa vibaya alipokuwa mtoto alipata kuelewa hekima ya maneno hayo. Anasema: “Kushiriki kwa ukaribu na kutaniko kulinisaidia kuwa na maoni mapya juu ya maisha. Haikuwa vigumu kuona kwamba wazee Wakristo walikuwa wenye upendo, nao walikuwa wachungaji wala si askari.” Naam, wazee Wakristo wenye huruma wanaweza kusaidia sana kuondosha hisia zisizofaa.—Isaya 32:1, 2; 1 Wathesalonike 2:7, 8.
-