Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuufanya Ulimwengu Uwe na Uraibu wa Dawa za Kulevya
    Amkeni!—1999 | Novemba 8
    • MTOTO mchanga aliyezaliwa hivi karibuni alia kwa sauti kubwa katika hospitali moja huko Madrid, Hispania. Muuguzi mmoja ajaribu kumtuliza kwa juhudi lakini bila mafanikio. Mtoto huyo anateseka kwa sababu ya kuacha kupewa heroini. Jambo lililo baya hata zaidi ni kwamba ana virusi vya HIV. Mama yake alikuwa mraibu wa heroini.

      Mama mmoja huko Los Angeles aendesha gari lake bila kujua kwenye barabara inayodhibitiwa na genge linalouza dawa za kulevya. Arushiwa risasi mfululizo, ambazo zamwua binti yake mchanga.

      Maelfu ya kilometa mbali na huko, katika Afghanistan, mkulima mmoja alima shamba la mmea unaotumika kutengenezea kasumba. Umekuwa mwaka wenye mazao; uzalishaji umeongezeka kwa asilimia 25. Mimea hiyo ya kasumba ina faida nyingi na familia ya mkulima huyo inajitahidi kujikimu. Lakini mimea hiyo mizuri itatumiwa kutengenezea heroini, na heroini huharibu maisha.

      Msichana mmoja mwenye haya huko Sydney, Australia, huenda kwenye disko kila Jumamosi usiku. Alikuwa akiona ugumu wa kuchangamana na umati, lakini hivi karibuni, tembe inayoitwa ecstasy imempa uhakika. Tembe anazotumia ziliingizwa Australia kwa njia ya magendo kutoka Uholanzi, ijapokuwa maabara za huko pia zimeanza kuzigawanya. Tembe ya ecstasy hufanya muziki uvutie zaidi, na kumfanya ashindwe kujizuia. Hata huhisi akiwa na sura nzuri zaidi.

      Kwa upande wa Manuel, mkulima hodari ambaye hupata riziki kwa taabu kutoka kwenye shamba lake dogo huko Andes, maisha yalikuwa afadhali alipoanza kulima koka. Manuel angependa kuacha kuvuna zao hilo, lakini anaogopa kwamba jambo hilo litawakasirisha wanaume wakatili wanaodhibiti uzalishaji wa koka katika eneo lake.

      Hawa ni baadhi ya watu wachache tu walioathiriwa na dawa za kulevya ambazo zinaharibu sayari yetu.a Iwe watu hawa ni wanunuzi, wazalishaji, au watu wasiojihusisha na wasiokuwa na hatia, dawa za kulevya zinadhibiti maisha yao daima.

      Tatizo la Dawa za Kulevya ni Kubwa Kadiri Gani?

      Katibu Mkuu wa UM Kofi Annan asema hivi: “Dawa za kulevya zinaharibu jamii zetu, zinaongeza uhalifu, zinaeneza maradhi kama vile UKIMWI, na kuua vijana wetu na kuharibu wakati wetu ujao.” Aongezea hivi: “Leo kuna watumiaji wa dawa za kulevya wanaokadiriwa kuwa milioni 190 ulimwenguni pote. Wako katika kila nchi. Na hakuna nchi yoyote kwa kujitegemea yenyewe, inayoweza kukomesha kwa mafanikio biashara ya dawa za kulevya katika mipaka yake. Biashara ya dawa za kulevya ambayo ni ya tufeni pote yahitaji itikio la kimataifa.”

      Jambo linalofanya hali iwe mbaya zaidi, ni kwamba katika miaka ya hivi majuzi, kumekuwako dawa za kulevyab za kubuniwa. Kemikali hizo za sanisia zimebuniwa kumfanya mtumiaji apumbae au ahisi furaha. Kwa kuwa dawa za kulevya za kubuniwa zinaweza kutengenezwa kwa bei rahisi karibu mahali popote, polisi hawana uwezo kabisa wa kuzidhibiti. Mnamo 1997, Tume ya Umoja wa Mataifa Inayoshughulika na Dawa za Kulevya ilionya kwamba katika nchi nyingi dawa hizi za kubuniwa zimekuwa sehemu ya “utamaduni wa watumiaji wengi” na kwamba zapasa kuonwa kuwa “tisho kubwa kwa jumuiya ya kimataifa katika karne ijayo.”

      Dawa za kulevya mpya zaidi ni zenye matokeo sawa na zile zilizotangulia. Kokeini iliyosafishwa hutokeza uraibu hata zaidi ya kokeini ya kawaida. Aina mpya za bangic zinatokeza njozi nyingi zaidi, na dawa mpya ya kulevya ya kubuniwa inayoitwa ice huenda ikawa miongoni mwa dawa zenye madhara makubwa zaidi.

      Pesa na Uwezo wa Dawa za Kulevya

      Ijapokuwa watumiaji wa dawa za kulevya huenda wakawa wachache, idadi yao inatosha kuwapa nguvu viongozi wa dawa za kulevya, watu wanaopanga uzalishaji na ugawaji wa dawa za kulevya. Watu hao wasio na maadili huendesha biashara ya ulaghai ambayo imekuwa yenye faida zaidi—na inakaribia kuwa biashara kubwa zaidi duniani. Biashara ya dawa za kulevya huenda sasa ikawa na mapato ya asilimia 8 ya biashara yote ya kimataifa, au takriban dola za Marekani 400,000,000,000 kila mwaka. Pesa zinazotokana na dawa za kulevya zinapozunguka ulimwenguni, zinatajirisha magenge, zinafisidi polisi, zinatumiwa kuhonga wanasiasa, na hata kulipia gharama za ugaidi.

  • Jinsi Ambavyo Dawa za Kulevya Haramu Huathiri Maisha Yako
    Amkeni!—1999 | Novemba 8
    • Pesa Zinazopatikana kwa Urahisi Kupitia Dawa za Kulevya—Kishawishi Kisichozuilika

      Je, wewe huhisi ukiwa salama katika ujirani wako baada ya giza kuingia? Ikiwa sivyo, labda ni kwa sababu ya wauzaji wa dawa za kulevya. Uvamizi na jeuri ya mitaani inahusiana sana na dawa za kulevya. Mara nyingi watumiaji wa dawa za kulevya hugeukia uhalifu au ukahaba ili kuendeleza zoea lao, huku magenge yenye kushindana yakipigana na kuuana ili kudhibiti ugawaji wa dawa za kulevya. Kwa kueleweka, polisi katika miji mingi huona dawa za kulevya kuwa zinachangia visa vingi vya uuaji ambavyo wanachunguza.

      Katika mabara fulani, waasi wameona faida za kutumia nguvu ili kujinufaisha na biashara yenye faida ya mihadarati. Kikundi kimoja cha waasi huko Amerika Kusini sasa kinajipatia nusu ya mapato yake kwa kuwalinda walanguzi wa dawa za kulevya. “Mapato yanayotokana na dawa za kulevya haramu hutumiwa kuendeleza baadhi ya mapambano makali zaidi ulimwenguni ya kidini na ya kikabila,” laripoti Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuzuia Ulanguzi wa Dawa za Kulevya Ulimwenguni.

  • Jinsi Ambavyo Dawa za Kulevya Haramu Huathiri Maisha Yako
    Amkeni!—1999 | Novemba 8
    • Ufisadi na Uchafu

      Ikiwa nyumba inaweza kudhoofishwa na ufisadi, hali kadhalika serikali zinaweza. Katika kisa hiki ni pesa za dawa za kulevya, badala ya dawa za kulevya zenyewe, ndizo hufisidi mfumo. “Dawa za kulevya zimefisidi maofisa wa serikali, polisi na jeshi,” akalalamika balozi mmoja kutoka nchi moja ya Amerika Kusini. Anaongezea kwamba pesa zinazopatikana ni “kishawishi kikubwa sana” kwa wale walio na tatizo la kujikimu.

      Nchi moja baada ya nyingine, mahakimu, mameya, polisi, na hata maofisa wa kupambana na ulanguzi wa dawa za kulevya wamenaswa katika hali ya ufisadi. Wanasiasa ambao huenda uchaguzi wao ulifanywa kwa kutumia pesa za viongozi wa ulanguzi wa dawa za kulevya hukataa wanapoombwa wachukue hatua kali za kinidhamu dhidi ya ulanguzi wa dawa za kulevya. Maofisa wengi wenye kufuatia haki ambao wameunga mkono kwa ujasiri harakati dhidi ya dawa za kulevya wameuawa.

      Hata udongo wetu, misitu yetu, na aina mbalimbali za viumbe wanaoishi humo wanateseka kutokana na pigo la tufeni pote la dawa za kulevya. Asilimia kubwa ya uzalishaji wa afyuni na kokeini hufanywa katika maeneo mawili ambayo yanaweza kupatwa na madhara ya kimazingira kwa urahisi: misitu ya mvua ya magharibi mwa Amazon na ile ya Kusini-mashariki ya Asia. Uharibifu katika sehemu hizo umekuwa mkubwa. Hata jitihada zenye kusifika za kuondoa mimea ya dawa za kulevya haramu huleta madhara makubwa kwa sababu ya dawa zinazotumika kuua mimea.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki