-
Kushinda Fadhaiko la DyslexiaAmkeni!—1996 | Agosti 8
-
-
Dyslexia Ni Nini?
Kamusi moja yafafanua dyslexia kuwa “kasoro ya uwezo wa kusoma.” Ingawa dyslexia huonwa kuwa tatizo la usomaji hiyo yaweza kutia ndani mengi zaidi.a
Asili ya neno la Kiingereza yatokana na Kigiriki dys, linalomaanisha “ugumu na,” na lexis, “neno.” Tatizo la Dyslexia latia ndani kupata magumu na maneno au lugha. Lahusisha pia matatizo ya kutoweza kuweka vitu kwa mfuatano ufaao, kama vile siku za juma na herufi katika neno. Kulingana na Dakt. H. T. Chasty, wa Taasisi ya Dyslexia ya Uingereza, dyslexia “ni kutoweza kuratibu kunakoathiri uwezo wa kukumbuka mambo yaliyotokea hivi punde, ufahamu na stadi za mkono.” Si ajabu kwamba wale wenye dyslexia hufadhaika sana!
Fikiria hali ya David. Ilikuwaje kwamba huyu mtu ambaye zamani alipenda sana kusoma na ambaye alikuwa msomaji mzuri sana akaja kuhitaji msaada wa mke wake wa kujifunza tena kusoma? Mshtuko wa akili uliharibu eneo fulani la ubongo wa David ambalo lilihusika na matumizi ya lugha, na jambo hilo lilifanya maendeleo yake ya kusoma kuwa polepole sana. Lakini, maneno marefu hayakumsumbua kama yale mafupi. Japo dyslexia aliyopata, uwezo wa David wa kuzungumza na akili yake timamu haikuathiriwa. Ubongo wa mwanadamu ni tata sana hivi kwamba watafiti hawajafahamu yote yanayohusika unaposhughulikia sauti na ishara za macho unazopokea.
Kwa upande mwingine Julie na Vanessa walikuwa na dyslexia ya kukua, ambayo ilikuja kuonekana wazi walipokuwa wakikua. Kwa ujumla watafiti hukubali kwamba watoto ambao kufikia umri wa miaka saba au nane na ambao wana akili za kawaida lakini wanapata magumu fulani ya kusoma, kuandika, na kuendeleza maneno huenda wakawa na dyslexia. Mara nyingi, vijana wenye dyslexia huziandika kinyume herufi wanazojaribu kunakili. Ebu wazia fadhaiko la Julie na Vanessa wakati walimu shuleni kwa makosa waliwaambia wao ni wajinga, wazito wa kujifunza, na wavivu!
-
-
Kushinda Fadhaiko la DyslexiaAmkeni!—1996 | Agosti 8
-
-
a Watu fulani wenye mamlaka hutumia neno “dysgraphia” kufafanua magumu ya kujifunza yanayohusiana na kuandika na pia “dyscalculia” kwa matatizo yahusikayo na hesabu.
-