Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kwa Nini Maisha Yanaonekana Kama Hayana Maana Yoyote?
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 1
    • Mungu Ana Kusudi Gani Kuelekea Dunia?

      Yehova Mungua aliiumba dunia ikiwa paradiso kamilifu—mahali ambapo wanaume na wanawake wangefurahia milele maisha kamili wakiwa wanadamu wakamilifu. Ukweli huo muhimu unapingana kabisa na wazo linalokubaliwa na wengi lakini lisilopatana na Maandiko kwamba Mungu aliiumba dunia iwe mahali ambapo angewajaribu wanadamu ili kuona kama wanastahili kuishi maisha yenye maana zaidi katika ulimwengu wa roho.—Ona sanduku “Je, Ni Lazima Tuondoke Duniani Ili Kufurahia Maisha Yenye Maana?” katika ukurasa wa 6.

      Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke kwa mfano wake, na kuwapa uwezo wa kuiga sifa zake nzuri. (Mwanzo 1:26, 27) Aliwaumba wakiwa wakamilifu. Walikuwa na kila kitu walichohitaji ili kufurahia maisha mazuri na yenye maana milele. Hilo lingetia ndani kuijaza dunia, kuitiisha, na kuibadilisha yote kuwa paradiso kama tu bustani ya Edeni.—Mwanzo 1:28-31; 2:8, 9.

  • Kwa Nini Maisha Yanaonekana Kama Hayana Maana Yoyote?
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 1
    • Kusudi la Mungu kuelekea dunia na wanadamu halijabadilika. Kupitia nabii Isaya, Yehova anatuhakikishia kuwa Yeye ndiye Mtengenezaji wa dunia, “ambaye hakuiumba tu bila sababu, ambaye aliiumba ili ikaliwe na watu.” (Isaya 45:18) Hivi karibuni, atairudisha dunia katika hali kamilifu aliyokusudia mwanzoni. Baada ya kuthibitisha kuwa njia yake ya kutawala ndiyo ya haki, atakuwa na sababu ya kutumia nguvu zake zisizo na kipimo kutimiza mapenzi yake na kuuondoa uovu wote. (Isaya 55:10, 11) Katika sala ya mfano, Yesu Kristo alimwomba Mungu achukue hatua hiyo. Yesu alitufundisha tusali hivi: “Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.” (Mathayo 6:9, 10) Hayo yanatia ndani nini?

      Mapenzi ya Mungu Kuelekea Dunia

      Kati ya baraka nyingine nyingi, “wapole wataimiliki dunia.” (Zaburi 37:9-11, 29; Methali 2:21, 22) Yesu Kristo “atamkomboa maskini anayelilia msaada, pia mwenye kuteseka.” Atawakomboa kutoka katika “ukandamizaji na katika jeuri.” (Zaburi 72:12-14) Hakutakuwa na vita tena; wala kifo, machozi, maumivu, au kuteseka. (Zaburi 46:9; Ufunuo 21:1-4) Maelfu ya watu ambao wamekufa wakati huu ambapo Mungu ameruhusu uovu uwepo, watafufuliwa waishi hapa duniani, na watakuwa na nafasi ya kufaidika na baraka hizo na nyinginezo.—Yohana 5:28, 29.

      Kwa kweli, Yehova ataondoa madhara yoyote ambayo yamesababishwa na uasi wa Shetani. Yehova atayaondoa kabisa hivi kwamba “taabu za zamani [mambo yote yanayosababisha majonzi na maumivu] kwa kweli zitasahauliwa.” (Isaya 65:16-19) Hatuna shaka yoyote kuhusu wakati huo ujao. Mungu hasemi uwongo. Ahadi zake zote zinatimia. Maisha hayatakuwa tena “ubatili na kufuatilia upepo.” (Mhubiri 2:17) Badala yake yatakuwa na maana tele.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki