-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Pia, mwezi wa Oktoba, watu 40 walikufa na wengine zaidi ya 100,000 wakalazimika kuhama makwao kwa sababu ya tetemeko kubwa la ardhi lililokumba eneo la kaskazini la Japani. Hakuna ndugu aliyejeruhiwa wala kufa, hata hivyo familia 200 ziliathiriwa na Jumba la Ufalme moja likaharibiwa kabisa. Tetemeko hilo lilipoanza wazee wa mzunguko wa eneo hilo walikuwa wamekusanyika ili kutayarisha kusanyiko la mzunguko. Wazee hao walifanyaje? Walifuata mwelekezo wa ofisi ya tawi na wa Halmashauri ya Ujenzi ya Mkoa ya eneo hilo, nao wakaanza mara moja kufanya mipango ya kutoa misaada. “Tulitiwa moyo tuwe na maoni ya kiroho kuhusu msiba huo,” anasema mzee fulani. Kusanyiko la mzunguko lilifanywa, na hata wale walioathiriwa na tetemeko hilo walihudhuria.
“Tetemeko hilo lilimtetemesha mume wangu,” anasema dada fulani ambaye mume wake si mwamini. Nyumba yao ilikuwa imeharibiwa. Alipoona jinsi ndugu walivyoonyesha upendo wakati wa kutoa misaada, mume huyo alihudhuria mkutano kwa mara ya kwanza. Alisema: “Naweza kulitegemea kabisa tengenezo lenu. Haliwezi kamwe kutukatisha tamaa.”
-
-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 20]
Ndugu wakisafisha Jumba la Ufalme lililoharibiwa na mafuriko katika Wilaya ya Niigata, Japani
-