Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Nina Tatizo la Kula?
    Amkeni!—2006 | Oktoba
    • Chukua Hatua Sasa!

      Hatua ya kwanza ni kukubali wewe binafsi kwamba una tatizo. “Baada ya kufikiria jambo hilo,” anasema Danielle, “niligundua nina hisia na mazoea kama ya wasichana walio na ugonjwa wa kujinyima chakula. Nilihofia kukubali kuwa nilikuwa nikifanya yaleyale waliyokuwa wakifanya.”

      Pili, sali kwa Yehova kuhusu tatizo lako.c Mwombe akusaidie kufahamu kinachosababisha tatizo lako ili ulishinde. Unaweza kusali hivi kama Daudi: “Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu. Unichunguze, na uzijue fikira zangu zinazofadhaisha, na uone kama ndani yangu mna njia yoyote yenye kuumiza, na uniongoze katika njia ya mpaka wakati usio na kipimo.”—Zaburi 139:23, 24.

      Kwa upande mwingine, huenda ukagundua kwamba unasita kuyaacha mazoea yako ya kula. Huenda yamekolea sana, yakawa kama uraibu. Unapaswa kusali kwa Yehova kuhusu jambo hilo. Danielle alihitaji kufanya hivyo hasa. “Mwanzoni,” anakubali, “sikutaka kushinda tatizo langu. Hivyo, nilihitaji kusali ili niwe na tamaa nzuri.”

      Tatu, zungumza na mzazi au mtu mwingine mzima anayeweza kukusaidia. Watu wazima wanaojali hawatakuaibisha. Badala yake, watajitahidi kumwiga Yehova, ambaye Biblia inasema hivi kumhusu: “Hakudharau wala kuchoshwa na mateso ya mwenye kuteseka; naye hakumficha uso wake, naye alipomlilia amsaidie alisikia.”—Zaburi 22:24.

      Kwa kweli, si rahisi kushinda tatizo hilo. Msaada wa wataalamu unahitajiwa katika visa fulani.d Lililo muhimu ni kuchukua hatua. Hilo ndilo jambo ambalo msichana mmoja, aliyekuwa na ugonjwa wa kula na kujitapisha, aliazimia kufanya. “Siku mmoja,” anasema, “nilitambua kwamba zoea la kujitapisha lilikuwa likinitawala. Lakini sikuwa na hakika kuwa ninaweza kulishinda. Hatimaye, nikafanya jambo gumu zaidi nililowahi kufanya. Niliomba msaada.”

      Unaweza kufanya vivyo hivyo!

  • Je, Nina Tatizo la Kula?
    Amkeni!—2006 | Oktoba
    • [Sanduku katika ukurasa wa 19]

      “Ninafikiri una tatizo ...”

      Mshiriki wa familia yako au rafiki akikuambia hivyo, epuka kujitetea. Tuseme rafiki yako amegundua kwamba nguo yako imeanza kufumuka upande wa nyuma. Je, hungemshukuru kwa kukujulisha kabla nguo yako haijafumuka kabisa? Biblia inasema: “Yuko rafiki anayeshikamana na mtu kwa ukaribu zaidi kuliko ndugu.” (Methali 18:24) Mtu fulani anapokutajia kuhusu tatizo ambalo huenda unalo, mtu huyo huwa rafiki wa aina hiyo!

  • Je, Nina Tatizo la Kula?
    Amkeni!—2006 | Oktoba
    • [Sanduku katika ukurasa wa 20]

      Ukitumbukia tena kwenye tatizo

      Unaweza kushinda mazoea yako ya kula, lakini uyarudie majuma au miezi kadhaa baadaye. Hilo likitukia, usife moyo. Biblia inakubali kwamba, “huenda mwadilifu akaanguka hata mara saba.” (Methali 24:16) Kuteleza si kuanguka. Badala yake, kunaonyesha tu uhitaji wa kuimarisha azimio lako, wa kutambua ishara zinazoonyesha unaelekea kurudia tena zoea lako, na wa kuzungumza tena waziwazi na mtu anayeweza kukutegemeza.

      [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 20]

      Soma kuhusu tatizo hilo

      Ikiwa una tatizo la kula, ingefaa usome kulihusu. Kadiri unavyoyajua ndivyo itakavyokuwa rahisi kukabiliana nayo. Huenda ukanufaika kusoma habari nzuri iliyo katika Amkeni! la Januari 22, 1999, ukurasa wa 3-12, na la Aprili 22, 1999, ukurasa wa 13-15.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki