Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kupatana juu ya Mahari ya Kiasi
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Septemba 15
    • Kanuni za Biblia Zenye Kupatana na Akili

      Iwapo wazazi Wakristo wataamua kufanya mapatano juu ya mahari au la ni uamuzi wa kibinafsi. Wakiamua kupatana, mapatano hayo yapaswa kufanywa kulingana na kanuni za Biblia. “Acheni namna yenu ya maisha iwe bila upendo wa fedha,” lasema Neno la Mungu. (Waebrania 13:5) Endapo kanuni hii haidhihiriki katika mapatano kuhusu ndoa, huenda mzazi Mkristo akawa anajidhihirisha kuwa kielelezo kisichofaa. Wanaume wenye madaraka katika kutaniko la Kikristo wapaswa kuwa wenye “kukubali sababu,” si ‘wapenda-fedha’ au “wenye pupa ya pato lisilo la haki.” (1 Timotheo 3:3, 8) Mkristo atozaye kiasi kikubwa cha mahari kwa pupa bila toba aweza hata kutengwa na ushirika wa kutaniko.—1 Wakorintho 5:11, 13; 6:9, 10.

  • Kupatana juu ya Mahari ya Kiasi
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Septemba 15
    • Ni Nani Apaswaye Kufanya Mapatano?

      Katika tamaduni fulani, huenda namna ambayo mapatano ya mahari hufanywa ikapingana kabisa na kanuni nyingine muhimu. Kulingana na Biblia, baba ndiye mwenye daraka juu ya mambo ya nyumba yake. (1 Wakorintho 11:3; Wakolosai 3:18, 20) Hivyo, wale wenye vyeo vyenye madaraka kutanikoni wapaswa kuwa wanaume wenye “[ku]simamia watoto na watu wa nyumbani mwao wenyewe kwa njia bora.”—1 Timotheo 3:12.

      Hata hivyo, huenda ikawa kawaida katika jamii kuacha mapatano ya muhimu ya ndoa yafanywe na watu wa jamaa ya kichwa cha familia. Na watu hao wa jamaa hudai kiasi fulani cha mahari. Hili hutahini nyumba za Kikristo. Wakidai kufuata desturi, vichwa fulani vya familia wameruhusu watu wa jamaa wasioamini kudai kiasi kikubwa sana cha mahari. Nyakati nyingine hili limefanya msichana Mkristo aolewe na mtu asiyeamini. Hilo lapingana na himizo la kwamba Mkristo apaswa kuoa au kuolewa “katika Bwana tu.” (1 Wakorintho 7:39) Kichwa cha familia anayewaruhusu watu wa jamaa yake wafanye maamuzi yenye kuhatarisha hali njema ya kiroho ya watoto wake, hawezi kuonwa kama “mwenye kusimamia nyumba yake vizuri.”—1 Timotheo 3:4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki