-
Kukirihi “Vitu Vyenye Kina Kirefu vya Shetani”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Wazee wanalinda waone miendo ya mielekeo isiyo ya kitheokrasi na utendaji makosa. Wanajaribu kusaidia wanaume na wanawake walio katika njia ya hatari ili hao wajenge hali ya kiroho na kurekebishwa kabla haijawa kuchelewa mno. (Wagalatia 5:16; 6:1) Kwa upendo na kwa uthabiti, waangalizi hawa Wakristo wanazuia jitihada yoyote ya kike ya kufanyiza vikundi vikundi vya kuendeleza miendo kama ile ya ukombozi wa wanawake. Zaidi ya hilo, pindi kwa pindi shauri la wakati wenye kufaa linatolewa katika vichapo vya Mashahidi wa Yehova.a
12. Ni kwa njia gani jamii ya Yohana leo inaonyesha bidii kama ile ya Yehu?
12 Hata hivyo, kunapokuwa na ukosefu wa adili mbaya sana, na hasa hilo linapokuwa ni zoea, watenda dhambi wasiotubu lazima watengwe na ushirika.
-
-
Kukirihi “Vitu Vyenye Kina Kirefu vya Shetani”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Wale ambao wameshindwa na uvutano huu wenye makosa wa kike pia watapatwa na dhiki kubwa—ile huzuni ya kutengwa na ushirika, kukatiliwa mbali na kundi la Kikristo kama kwamba ni wafu. Isipokuwa hawa wanatubu, wanageuka, na wanakubaliwa tena ndani ya kundi, wanakabili pia kifo cha kimwili kwa “tauni yenye kufisha”—mwishowe kabisa, katika ile dhiki kubwa. Kwa wakati huu, kurudishwa kunawezekana ikiwa wanatubia kabisa matendo yao yenye kosa.—Mathayo 24:21, 22; 2 Wakorintho 7:10.
14. (a) Yesu anatumiaje wazee katika kushughulikia matatizo fulani, kama vile uvutano wowote wa Kiyezebeli? (b) Imelipasa kundi liungeje mkono wazee wanaoshughulikia matatizo kama hayo?
14 “Makundi yote” lazima yaje kujua kwamba Yesu anachunguza “figo,” zile hisia zenye kina kirefu zaidi sana, na ‘moyo,’ yule mtu wa ndani-ndani zaidi, kutia na makusudio yaliyo chinichini. Kutimiza hilo, yeye anatumia nyota, au wazee wenye kuitibarika, katika kushughulikia matatizo fulani fulani, kama vile uvutano wowote wa Kiyezebeli unaotokea. (Ufunuo 1:20, NW) Baada ya hawa wazee kuchunguza kikamili jambo fulani la aina hii na hukumu imekwisha pitishwa, si juu ya watu mmoja mmoja kuchungua-chungua ni kwa sababu gani na kwa nini hatua ilichukuliwa vile. Wote wamepaswa kukubali kwa unyenyekevu kumalizwa kwa mambo na wazee na kuendelea kuunga mkono nyota hizi za kundi. Ushikamanifu kwa Yehova na kwa mipango yake ya kitengenezo utathawabishwa. (Zaburi 37:27-29; Waebrania 13:7, 17)
-