Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuthamini “Zawadi Zikiwa Wanadamu”
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Juni 1
    • ‘Sisi Ni Wafanyakazi Wenzenu’

      4, 5. (a) Paulo analifananisha kutaniko na nini, na kwa nini kielezi hicho chafaa? (b) Kielezi cha Paulo kinaonyesha nini kuhusiana na jinsi tunavyopaswa kuwaona na kuwatendea wenzetu?

      4 Yehova amewakabidhi “zawadi zikiwa wanadamu” kiasi fulani cha mamlaka kutanikoni. Bila shaka, wazee hawangependa kutumia vibaya mamlaka yao, ingawa wao wanajua kuwa ni rahisi sana kwa wanadamu wasiokamilika kufanya hivyo. Basi, wao wanapaswa kujionaje kuhusiana na washiriki wengine wa kundi? Fikiria kielezi ambacho mtume Paulo alitumia. Akiisha kuzungumzia sababu ya kuandaliwa kwa “zawadi zikiwa wanadamu,” Paulo aliandika hivi: “Na tukue kwa upendo katika mambo yote katika yeye aliye kichwa, Kristo. Kutoka katika yeye mwili wote, kwa kuunganishwa pamoja kwa upatano na kufanywa ushirikiane kupitia kila kiungo ambacho hupa kile kihitajiwacho, kulingana na utendaji wa kila kiungo kimoja-kimoja katika kipimo kipasacho, hutokeza ukuzi wa mwili ili kujijenga huo wenyewe katika upendo.” (Waefeso 4:15, 16) Hivyo Paulo alilifananisha kutaniko, pamoja na wazee na washiriki wengine, na mwili wa binadamu. Kwa nini kielezi hicho chafaa?

      5 Mwili wa binadamu una viungo vingi mbalimbali lakini una kichwa kimoja pekee. Hata hivyo, hakuna chochote mwilini—kiwe ni msuli, neva, au mshipa wa damu—ambacho hakifai. Kila kiungo ni muhimu, nacho huchangia jambo fulani kwa afya na uzuri wa mwili wote. Vivyo hivyo, kutaniko limefanyizwa na washiriki mbalimbali, lakini kila mmoja—wachanga kwa wazee, wenye nguvu au wenye udhaifu—anaweza kuchangia jambo fulani kwa afya ya kiroho na uzuri wa kutaniko kwa ujumla. (1 Wakorintho 12:14-26) Yeyote asione kuwa hafai chochote. Kwa upande mwingine wenye kupita kiasi, yeyote asijione kuwa bora, kwa kuwa sisi sote—wachungaji na kondoo vilevile—ni sehemu ya mwili, na kuna kichwa kimoja tu, Kristo. Hivyo Paulo atoa mfano mzuri wa upendo, kujali, na staha tunazopaswa kuonyeshana. Kutambua jambo hilo kunawasaidia wazee kuwa na maoni ya unyenyekevu na yenye usawaziko juu ya daraka lao kutanikoni.

      6. Ingawa Paulo alikuwa na mamlaka ya kimitume, yeye alionyeshaje roho ya unyenyekevu?

      6 Hao “zawadi zikiwa wanadamu” hawatafuti kudhibiti maisha au imani ya waabudu wenzao. Ingawa Paulo alikuwa na mamlaka ya kimitume, kwa unyenyekevu aliwaambia Wakorintho hivi: “Si kwamba sisi ndio mabwana-wakubwa juu ya imani yenu, bali sisi ni wafanyakazi wenzi kwa shangwe yenu, kwa maana ni kwa imani yenu kwamba nyinyi mnasimama.” (2 Wakorintho 1:24) Paulo hakutaka kudhibiti imani na njia ya maisha ya ndugu zake. Kwa hakika hakuona uhitaji wa kufanya hivyo, kwa kuwa alionyesha uhakika kwamba tayari walikuwa wanaume na wanawake waaminifu waliokuwa katika tengenezo la Yehova kwa sababu walitaka kufanya yaliyo mema. Kwa hiyo, akisema kujihusu mwenyewe na kumhusu mwandamani wake Timotheo, kwa kweli Paulo alikuwa akimaanisha hivi: ‘Ni wajibu wetu kuwasaidia nyinyi mmtumikie Mungu kwa shangwe.’ (2 Wakorintho 1:1) Hiyo ilikuwa roho ya unyenyekevu kama nini!

      7. Wazee wanyenyekevu hutambua nini kuhusu daraka lao kutanikoni, nao wana uhakika upi na wafanyakazi wenzao?

      7 Leo, “zawadi zikiwa wanadamu” wana wajibu huohuo. Wao ni ‘wafanyakazi wenzi kwa shangwe yetu.’ Wazee wanyenyekevu hutambua kwamba si juu yao kuamua kiasi ambacho wengine wanaweza kufanya katika utumishi kwa Mungu. Wanajua kuwa ingawa huenda wakawatia wengine moyo wapanue au kuboresha huduma yao, utumishi kwa Mungu unapasa kutoka ndani ya moyo wenye kupenda. (Linganisha 2 Wakorintho 9:7.) Wao wana uhakika kuwa ikiwa wafanyakazi wenzao wana shangwe, watafanya kadiri wawezavyo. Kwa njia hiyo wao wana tamaa kubwa ya kuwasaidia ndugu zao ‘wamtumikie BWANA kwa furaha.’—Zaburi 100:2.

  • Kuthamini “Zawadi Zikiwa Wanadamu”
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Juni 1
    • 9. Ni maoni gani kuhusu wazee wengine yatakayomsaidia kila mzee kutumikia kwa shangwe?

      9 Kuwa na maoni yenye unyenyekevu kwamba wewe ni ‘mfanyakazi mwenzi’ kutakusaidia wewe kutumikia kwa shangwe na kuzithamini zawadi za pekee za wazee wenzako. Kila mzee ana vipaji na uwezo wake mwenyewe anavyoweza kutumia kwa faida ya kutaniko. (1 Petro 4:10) Huenda mzee mmoja ana zawadi ya kufundisha. Huenda mwingine akawa ana uwezo wa kuratibu mambo. Na bado huenda mwingine akawa mwenye kufikiwa kwa urahisi zaidi kwa sababu ya uchangamfu wake na huruma zake. Ukweli ni kwamba hakuna mzee aliye na kila zawadi kwa kiwango kilekile. Je, kuwa na zawadi fulani hususa—kwa mfano, zawadi ya kufundisha—humfanya mzee mmoja kuwa bora kuliko mwingine? La, hasha! (1 Wakorintho 4:7) Kwa upande mwingine, hakuna haja kuhusudu zawadi ambayo mwingine anayo au kuona kuwa hufai wakati mzee mwingine anapopongezwa na wengine kwa sababu ya uwezo wake. Kumbuka kuwa wewe mwenyewe una zawadi ambazo Yehova huziona ndani yako. Naye anaweza kukusaidia kuzisitawisha zawadi hizo na kuzitumia kwa faida ya ndugu zako.—Wafilipi 4:13.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki