-
Je, Waogopa Kuwa na Itibari Katika Wengine?Mnara wa Mlinzi—1997 | Machi 1
-
-
Katika yale makutaniko zaidi ya 80,000 ya Mashahidi wa Yehova duniani pote, kuna wanaume wanyenyekevu wanaotumikia wakiwa “wafanyakazi wenzi kwa shangwe yenu.” (2 Wakorintho 1:24) Hao ni wazee. “[“Kila mmoja,” NW],” asema Isaya “atakuwa kama mahali pa kujificha na upepo, na mahali pa kujisitiri na dhoruba; kama mito ya maji mahali pakavu, kama kivuli cha mwamba mkubwa katika nchi yenye uchovu.” Hivyo ndivyo wazee hujitahidi kuwa.—Isaya 32:2; 50:4; 1 Wathesalonike 5:14.
Wazee hutimiza matakwa ya Kimaandiko kabla ya ‘roho takatifu kuwaweka rasmi.’ Kujua hilo kutaimarisha uhakika wako katika wao. (Matendo 20:28; 1 Timotheo 3:2-7; Tito 1:5-9) Yale unayozungumza pamoja na mzee yatabaki siri kabisa. Sifa moja ya ustahili wake ni kuwa mwenye kutumainika.—Linganisha Kutoka 18:21; Nehemia 7:2.
Wazee kutanikoni “wanafuliza kulinda juu ya nafsi zenu kama wale watakaotoa hesabu.” (Waebrania 13:17) Je, hilo halikusukumi uweke itibari yako katika wanaume hao? Kwa asili, si wazee wote walio bora katika sifa zilezile. Huenda wazee fulani wakaonekana kuwa wenye kufikika zaidi, wenye fadhili, au wenye uelewevu kuliko wengine. (2 Wakorintho 12:15; 1 Wathesalonike 2:7, 8, 11) Kwa nini usifunue mambo ya siri kwa mzee ambaye wahisi kuwa starehe naye?
Wanaume hao si wafanyakazi wa kitaaluma wanaolipwa mshahara. Badala ya hivyo, wao ni “zawadi zikiwa wanadamu,” walioandaliwa na Yehova ili kukusaidia. (Waefeso 4:8, 11-13; Wagalatia 6:1) Jinsi gani? Kwa kuitumia Biblia kwa ustadi, watatumia nguvu zayo za kuponya katika hali yako binafsi. (Zaburi 107:20; Mithali 12:18; Waebrania 4:12, 13) Watasali pamoja nawe na kwa ajili yako. (Wafilipi 1:9; Yakobo 5:13-18) Msaada kutoka kwa washauri hao wenye upendo waweza kuchangia sana katika kuponya roho yenye usumbufu na kurudisha amani ya akilini.
-
-
Je, Waogopa Kuwa na Itibari Katika Wengine?Mnara wa Mlinzi—1997 | Machi 1
-
-
Waweza kujifunzaje kuwa na itibari katika wazee na wengine kutanikoni? Kwanza, jichunguze mwenyewe. Je, hofu zako zina msingi thabiti? Je, wewe watilia shaka nia za wengine? (1 Wakorintho 13:4, 7) Je, kuna njia ya kupunguza hatari za kuumizwa? Ndiyo. Jinsi gani? Katika kikao cha kiroho, jaribu kufahamiana na wale unaotaka kuwafunulia mambo ya siri. Zungumza nao kwenye mikutano ya kutaniko. Shiriki pamoja nao katika mahubiri ya nyumba hadi nyumba. Sawa na staha, lazima itibari ichumwe. Kwa hiyo uwe na subira. Kwa kielelezo, upatapo kumjua kuwa mchungaji wa kiroho, uhakika wako kwake, utaongezeka. Funua mahangaiko yako hatua kwa hatua. Akiitikia kwa njia ifaayo, yenye huruma, na ya busara, waweza basi kujaribu kufunua mambo mengine.
Waabudu wenzako wa Yehova, hasa wazee Wakristo, hujitahidi kuiga sifa za Mungu zenye kupendekeza katika mahusiano ya wao kwa wao. (Mathayo 5:48) Hilo latokeza mazingira ya itibari kutanikoni. Mmoja ambaye amekuwa mzee kwa muda mrefu asema hivi: “Lazima ndugu wajue jambo moja: Liwe ni jambo gani mtu afanya, mzee hapotezi upendo wake wa Kikristo kumwelekea mtu huyo. Huenda asipende jambo lililofanywa, lakini bado ampenda ndugu yake na ataka kumsaidia.”
-