Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kukabili Mtihani wa Uaminifu-Mshikamanifu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Machi 15
    • Uaminifu-Mshikamanifu kwa Wazee Waaminifu-Washikamanifu

      11. Uaminifu-mshikamanifu utatulinda dhidi ya fikira gani hasi?

      11 Jambo fulani lisemwapo au kufanywa kutanikoni ambalo hatuelewi vizuri, uaminifu-mshikamanifu utatuzuia tusihukumu-hukumu mambo nao utatusaidia kuona kwamba labda hilo ni jambo la uamuzi. Je, si afadhali sana kufikiria sifa nzuri za wazee waliowekwa rasmi kutanikoni na waamini wenzetu wengine badala ya kufikiria mapungufu yao? Ndiyo twataka kulinda dhidi ya fikira hasi kama hizo, kwa kuwa zinahusiana na kukosa uaminifu-mshikamanifu! Uaminifu-mshikamanifu pia utatusaidia kutii mwelekezo wa Paulo wa ‘kutosema kwa ubaya juu ya yeyote.’—Tito 3:1, 2, NW.

  • Kukabili Mtihani wa Uaminifu-Mshikamanifu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Machi 15
    • 14, 15. Ni mambo gani yawezayo kutahini uaminifu-mshikamanifu wa washiriki wa kutaniko?

      14 Kuna pande nyinginezo za suala la kukabili mtihani wa uaminifu-mshikamanifu kwa kutaniko na wazee walo. Iwapo kwa njia fulani kuna matatizo katika kutaniko, hilo hutupa fursa ya kuonyesha uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova na kwa wale wanaomwakilisha. (Ona Mnara wa Mlinzi, Juni 15, 1987, kurasa 15-17.) Ikiwa mtu ametengwa na ushirika, uaminifu-mshikamanifu wataka kwamba tuunge mkono wazee, si kujaribu kufikiria kama kulikuwa na sababu za kutosha zilizofanya hatua hiyo ichukuliwe.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki