Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tianeni Nguvu
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Mei 1
    • Isitoshe, tunahitaji kuwa wanyenyekevu kukubali kwamba huenda nyakati nyingine tukahitaji kusaidiwa tunapopatwa na shida. Paulo alikiri kwamba alihitaji msaada na kuukubali kwa upole huku akiwapongeza walioutoa. Hakuona ni udhaifu au ni aibu kukubali msaada kutoka kwa wengine, nasi pia tunapaswa kuwa vivyo hivyo. Tukisema kwamba hatuhitaji msaada wenye kutia nguvu, hiyo itamaanisha tuna nguvu zinazozidi za binadamu. Kumbuka kwamba mfano wa Yesu unaonyesha kuwa huenda wakati mwingine hata mwanadamu mkamilifu akalilia msaada.—Waebrania 5:7.

      9, 10. Kunaweza kuwa na matokeo gani mazuri mtu akikubali kwamba anahitaji msaada, na jambo hilo linaweza kuathirije washiriki wengine katika familia na kutanikoni?

      9 Matokeo yanaweza kuwa mazuri iwapo ndugu wenye madaraka watakubali kwamba wamepungukiwa na kwamba wanategemea msaada wa wengine. (Yakobo 3:2) Kufanya hivyo huimarisha uhusiano kati ya wale walio na madaraka na wale walio chini yao, na hivyo kukuza mawasiliano yenye uchangamfu na ya kirafiki. Unyenyekevu wa wale wanaokubali msaada unakuwa mfano halisi kwa wale walio katika hali kama hiyo. Hiyo huonyesha kwamba wenye kuongoza ni wanadamu wanaoweza kufikika.—Mhubiri 7:20.

  • Tianeni Nguvu
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Mei 1
    • Vivyo hivyo, washiriki wa kutaniko watakuwa tayari zaidi kukubali msaada kutoka kwa wazee wanapotambua kwamba wazee pia hukabili matatizo, hofu, na mambo yenye kutatanisha. (Waroma 12:3; 1 Petro 5:3) Pia, kunaweza kuwa na mawasiliano mazuri, mashauri kutoka katika Maandiko yanaweza kuzungumziwa, na imani inaweza kuimarishwa. Kumbuka kwamba ndugu na dada zetu wanahitaji kuimarishwa hasa wakati huu.—2 Timotheo 3:1.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki