Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mume na Mzee—Kusawazisha Hayo Madaraka
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Oktoba 15
    • Kuwa Mzee na Ndoa Ni Mambo Yanayopatana

      3. Ni mambo gani ya hakika ya Kimaandiko yaonyeshayo kwamba waangalizi Wakristo waweza kuwa wanaume waliooa?

      3 Badala ya kutaka kwamba wanaume waliowekwa rasmi wawe waangalizi wasioe, Paulo alimwandikia Tito hivi: “Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee [Kigiriki, pre·sbyʹte·ros] katika kila mji kama vile nilivyokuamuru; ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii. Maana imempasa askofu [“mwangalizi,” NW] [Kigiriki, e·piʹsko·pos, litokapo neno “askofu”] awe mtu asiyeshitakiwa neno, kwa kuwa ni wakili wa Mungu.”—Tito 1:5-7.

      4. (a) Twajuaje kwamba ndoa si takwa kwa waangalizi Wakristo? (b) Ndugu mseja aliye mzee ana faida gani?

      4 Kwa upande mwingine, ndoa si takwa la Kimaandiko la kuwa mzee. Yesu alidumu akiwa mseja. (Waefeso 1:22) Paulo, mwangalizi mwenye kutokeza katika kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza, alikuwa asiyeoa wakati huo. (1 Wakorintho 7:7-9) Leo, kuna Wakristo wengi waseja wanaotumikia wakiwa wazee. Hali yao ya useja labda huwaruhusu wawe na wakati mwingi zaidi kushughulikia wajibu wao mbalimbali wakiwa waangalizi.

  • Mume na Mzee—Kusawazisha Hayo Madaraka
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Oktoba 15
    • 10. Ili Mkristo astahili kuwa mzee, ndugu zake na watu walio nje wapaswa kuweza kuona nini?

      10 Ingawa ndoa si takwa la kuwa mzee, ikiwa mwanamume Mkristo alioa, kabla ya kupendekezwa kwa ajili ya kuwekwa rasmi kuwa mzee, kwa hakika apaswa kutoa uthibitisho wa kujitahidi kuwa mume mwema, mwenye upendo, huku akitumia ukichwa ifaavyo. (Waefeso 5:23-25, 28-31) Paulo aliandika hivi: “Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu [“mwangalizi,” NW], atamani kazi njema. Basi imempasa askofu [“mwangalizi,” NW] awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja.” (1 Timotheo 3:1, 2) Yapaswa iwe dhahiri kwamba mzee anafanya kadiri awezavyo ili kuwa mume mwema, mke wake awe ni Mkristo mwenzake au la. Kwa kweli, hata watu walio nje ya kutaniko wapaswa kuweza kuona kwamba anamtunza mke wake vizuri na yale madaraka yake mengine. Paulo aliongeza hivi: “Imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.”—1 Timotheo 3:7.

      11. Fungu la maneno “mume wa mke mmoja” ladokeza nini, kwa hiyo wazee wachukue hatua zipi za kujihadhari?

      11 Bila shaka, fungu la maneno “mume wa mke mmoja” lakataza ndoa ya wake wengi, na pia ladokeza uaminifu wa ndoa. (Waebrania 13:4) Wazee wahitaji hasa kuwa waangalifu wanaposaidia dada kutanikoni. Wapaswa kuepuka kuwa peke yao wanapomtembelea dada fulani anayehitaji shauri na faraja. Wangefanya vema kuandamana na mzee mwingine, mtumishi wa huduma, au hata mke wao ikiwa ni jambo la kufanya ziara ya kutia moyo tu.—1 Timotheo 5:1, 2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki