Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wasaidieni Kondoo Waliopotea
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
    • 15 Tuseme wewe ni mzee na unafanya ziara ya uchungaji. Unaweza kuwatia moyo wenzi wa ndoa wasiotenda wakumbuke wakati ambapo walijifunza kweli ya Neno la Mungu kwa mara ya kwanza. Kweli ilikuwa nzuri ajabu, ilieleweka wazi, iliridhisha, na iliwaweka huru kiroho! (Yoh. 8:32) Mioyo yao ilijaa shukrani kwa sababu ya mambo ambayo walikuwa wakijifunza kumhusu Yehova, upendo wake, na makusudi yake bora! (Linganisha na Luka 24:32.) Wakumbushe kwamba Wakristo waliojiweka wakfu wanafurahia uhusiano wa karibu pamoja na Yehova na pendeleo zuri la sala. Fanya yote unayoweza kuwatia moyo wasiotenda wakubali tena “habari njema yenye utukufu ya Mungu mwenye furaha,” Yehova.—1 Tim. 1:11.

  • Wasaidieni Warudi Haraka!
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
    • 2. Ni jambo gani tunalopaswa kukumbuka kuhusu mambo ya siri au ya kihukumu?

      2 Yehova aliwahangaikia kondoo waliopotea wa Israeli. (Soma Ezekieli 34:15, 16.) Vivyo hivyo, wazee Wakristo wanataka na wana wajibu wa kumsaidia mtu aliye kama kondoo ambaye ameacha kushirikiana na kundi.

  • Wasaidieni Warudi Haraka!
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
    • Je, “Mahangaiko ya Maisha” Yamepunguza Bidii Yao?

      5, 6. (a) Kwa nini ni jambo la maana tusikilize kwa makini waamini wenzetu wasiotenda wanapotueleza hisia zao? (b) Unaweza kuwasaidia jinsi gani wasiotenda waone kwamba wamepata hasara kwa kutoshirikiana na watu wa Mungu?

      5 Ili kujua jinsi ambavyo watawasaidia waamini wenzao wasiotenda, wazee na wahubiri wengine wakomavu wanahitaji kusikiliza kwa makini wakati watu hao wasiotenda wanapoeleza hisia zao. Tuseme wewe ni mzee na umewatembelea wenzi wa ndoa ambao wameacha kushirikiana na kutaniko kwa sababu ya “mahangaiko ya maisha.” (Luka 21:34) Huenda matatizo ya kifedha au madaraka ya familia yameongezeka na kuwafanya wawe wasiotenda kiroho. Labda wanahisi kwamba wanahitaji kupumzika kiroho, lakini unaweza kuwaeleza kwamba suluhisho si kujitenga na wengine. (Soma Methali 18:1.) Unaweza kuwauliza hivi kwa busara: “Je, mmepata furaha zaidi tangu mlipoacha kuhudhuria mikutano? Je, familia yenu imefanikiwa zaidi? Je, bado shangwe ya Yehova ni ngome yenu?”—Neh. 8:10.

      6 Kutafakari kuhusu maswali hayo kunaweza kuwasaidia wasiotenda kuona kwamba kwa sababu ya kuacha kushirikiana na kutaniko, hali yao ya kiroho na furaha yao imepungua. (Mt. 5:3; Ebr. 10:24, 25) Unaweza kuwasaidia kuona kwamba shangwe yao imepungua pia kwa sababu ya kuacha kuhubiri habari njema. (Mt. 28:19, 20) Hivyo basi, ni hatua gani ya hekima wanayopaswa kuchukua?

      7. Tunaweza kuwatia moyo wale walioacha kushirikiana na kundi wafanye nini?

      7 Yesu alisema hivi: “Jiangalieni ninyi wenyewe kwamba mioyo yenu isilemewe kamwe na kula kupita kiasi na kunywa sana na mahangaiko ya maisha . . . Endeleeni kukesha wakati wote mkiomba dua ili mpate kufanikiwa kuponyoka mambo yote hayo yaliyokusudiwa kutukia.” (Luka 21:34-36) Wale ambao wameacha kushirikiana na kundi na wanataka tena kupata furaha wanaweza kutiwa moyo kusali kwa ajili ya roho takatifu na msaada kutoka kwa Mungu na kutenda kupatana na sala zao.—Luka 11:13.

      Je, Walikwazwa?

      8, 9. Mzee anaweza kumsaidia jinsi gani mtu aliyekwazwa?

      8 Kwa kuwa wanadamu si wakamilifu, nyakati nyingine wanaweza kukosana, na mmoja wao anaweza kukwazika. Wengine wamekwazwa kwa sababu mtu mwenye kuheshimika katika kutaniko hakufuata kanuni za Biblia. Ikiwa mtu asiyetenda amekwazwa kwa sababu hiyo, mzee ambaye amemtembelea anaweza kutaja kwamba Yehova hamkwazi mtu yeyote. Kwa hiyo, kwa nini mtu avunje uhusiano wake pamoja na Mungu na watu Wake? Badala yake, anapaswa kuendelea kumtumikia Mungu, na kuwa na uhakika kwamba “Mwamuzi wa dunia yote” anajua mambo yaliyotendeka na atayashughulikia kwa njia inayofaa. (Mwa. 18:25; Kol. 3:23-25) Mtu akijikwaa kihalisi na kuanguka, hawezi kuendelea kukaa chini bila hata kujaribu kusimama.

      9 Katika jitihada zake za kutoa msaada wa kiroho, mzee anaweza kutaja kwamba baada ya muda, watu fulani wanagundua kwamba mambo yaliyowafanya wakwazike si ya maana sana kama walivyoyaona mbeleni. Na kwa kweli, huenda hali iliyowakwaza haipo tena. Ikiwa mtu alikwazika kwa sababu alitiwa nidhamu, kusali na kutafakari kunaweza kumfanya atambue kwamba yeye mwenyewe alikosea kwa kadiri fulani na kwamba hakupaswa kuruhusu nidhamu imkwaze.—Zab. 119:165; Ebr. 12:5-13.

      Je, Walikwazwa na Fundisho Fulani?

      10, 11. Ni hoja gani zinazoweza kumsaidia mtu ambaye alielewa fundisho fulani la Biblia kwa njia tofauti?

      10 Huenda wengine waliliacha kundi la Mungu kwa sababu hawakukubaliana na fundisho fulani la Biblia. Waisraeli waliowekwa huru kutoka utekwani huko Misri ‘walisahau kazi’ ambazo Mungu alifanya kwa ajili yao, nao “hawakungojea shauri lake.” (Zab. 106:13) Unaweza kumsaidia mtu asiyetenda kwa kumkumbusha kwamba “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ndiye anayeandaa chakula bora cha kiroho. (Mt. 24:45) Hivyo ndivyo mtu huyo alivyojifunza kweli. Kwa hiyo, kwa nini asiazimie kutembea tena katika kweli?—2 Yoh. 4.

      11 Anapojitahidi kuwasaidia wale ambao wameacha kushirikiana na kundi la Mungu, mzee anaweza kuzungumzia jinsi wanafunzi walivyomwacha Yesu kwa sababu walikataa jambo fulani ambalo alifundisha. (Yoh. 6:53, 66) Walipoacha kushirikiana na Kristo na wafuasi wake waaminifu, hawakuthamini tena mambo ya kiroho nao wakapoteza shangwe yao. Je, wale ambao wameacha kushirikiana na kutaniko la Kikristo wamepata mahali pengine penye chakula kingi cha kiroho? Hapana, kwa maana hakuna pengine!

      Je, Walifanya Dhambi Nzito?

      12, 13. Mtu aliyeacha kushirikiana na kundi akikubali kwamba ametenda dhambi nzito, anaweza kusaidiwa jinsi gani?

      12 Watu fulani wanaacha kuhubiri na kuhudhuria mikutano kwa sababu wamefanya dhambi nzito. Huenda wakahisi kwamba wakiungama dhambi yao kwa wazee, watatengwa na ushirika. Lakini hawawezi kutengwa na ushirika wa kutaniko ikiwa wameacha zoea hilo lisilopatana na Maandiko na ikiwa wametubu kikweli. (2 Kor. 7:10, 11) Badala yake, watakaribishwa tena, na wazee watawapa msaada wa kiroho ambao wanahitaji.

  • Wasaidieni Warudi Haraka!
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Novemba 15
    • “Mwanangu, Karibu Nyumbani!”

      16-18. (a) Mzee mmoja Mkristo alimsaidia jinsi gani ndugu fulani ambaye kwa miaka mingi alikuwa asiyetenda? (b) Ni nini kilichomfanya ndugu huyo awe asiyetenda, na kutaniko lilimpokea jinsi gani?

      16 Mzee mmoja Mkristo alisema hivi: “Baraza letu la wazee linajitahidi sana kuwatembelea wasiotenda. Pindi moja, nilimkumbuka ndugu fulani ambaye nilijifunza Biblia pamoja naye na kumsaidia kupata ujuzi wa kweli. Alikuwa mhubiri asiyetenda kwa miaka 25 hivi naye alikuwa akikabili hali ngumu sana, hivyo nilimweleza jinsi kufuata kanuni za Biblia kunavyoweza kumsaidia. Baada ya muda fulani, alianza kuja kwenye Jumba la Ufalme naye akakubali kujifunza Biblia ili aimarishe azimio lake la kurudi katika kundi.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki