-
Maisha Yenye Kuridhisha Katika Ulimwengu Mpya wa MunguMnara wa Mlinzi—2006 | Februari 1
-
-
Maisha Yenye Kuridhisha Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu
DAVID,a mume Mkristo ambaye pia ni baba, alihamia Marekani, akiwa na uhakika kwamba alikuwa amefanya uamuzi unaofaa. Ingawa hakufurahia kuacha mke na watoto wake, alikuwa na uhakika kwamba angeboresha maisha yao ikiwa angepata pesa zaidi. Hivyo, alikubali mwaliko wa watu wa ukoo huko New York na punde si punde akapata kazi huko.
Hata hivyo, kadiri muda ulivyopita, David alianza kukata tamaa. Hakuwa na wakati wa kutosha kwa ajili ya mambo ya kiroho. Hata wakati fulani karibu aache kumwamini Mungu. Aligundua uhalisi wa mambo alipoanguka katika kishawishi. Hatua kwa hatua, kufuatia utajiri wa kimwili kukamfanya aanze kupuuza vitu vyote vilivyokuwa muhimu kwake. Alihitaji kufanya mabadiliko.
Kama David, watu wengi huhama nchi maskini kila mwaka wakitumaini kuboresha hali yao ya kiuchumi. Hata hivyo, mara nyingi hali yao ya kiroho huzorota. Baadhi yao wamejiuliza, ‘Je, Mkristo anaweza kufuatia utajiri wa kimwili na wakati uleule awe tajiri kumwelekea Mungu?’ Waandishi na viongozi wa kidini wanaojulikana sana husema kwamba inawezekana. Lakini David na wengine wametambua kwamba si rahisi kuwa na mali na wakati uleule kudumisha maadili.—Luka 18:24.
-
-
Maisha Yenye Kuridhisha Katika Ulimwengu Mpya wa MunguMnara wa Mlinzi—2006 | Februari 1
-
-
Pili, kama David aliyetajwa mwanzoni alivyogundua, mara nyingi kufuatia utajiri huchukua wakati mwingi na nguvu nyingi za mtu hivi kwamba pole kwa pole anaacha kufuatia mambo ya kiroho. (Luka 12:13-21)
-
-
Maisha Yenye Kuridhisha Katika Ulimwengu Mpya wa MunguMnara wa Mlinzi—2006 | Februari 1
-
-
David alikuwa karibu kupoteza familia yake, imani yake, na uhusiano wake pamoja na Mungu. Hata hivyo, alirekebisha maisha yake. Kama Yesu alivyoahidi, David alipoanza tena kutanguliza kujifunza Biblia, kusali, na kuhubiri, mambo mengine yakawa shwari. Hatua kwa hatua, uhusiano wake pamoja na mke na watoto wake uliboreka. Akapata tena shangwe na uradhi. Bado anafanya kazi kwa bidii. Ingawa hakupata utajiri, kisa chake chenye kuhuzunisha kilimfunza mambo muhimu.
David ametambua kwamba halikuwa jambo la hekima kuhamia Marekani, naye ameazimia kutoruhusu tena pesa ziongoze maamuzi yake. Sasa anajua kwamba vitu vyenye thamani zaidi maishani, yaani, familia yenye upendo, rafiki wazuri, na uhusiano pamoja na Mungu, haviwezi kununuliwa kwa pesa. (Methali 17:17; 24:27; Isaya 55:1, 2) Bila shaka, kufuatia maadili ni jambo lenye thamani sana kuliko utajiri. (Methali 19:1; 22:1) David na familia yake wameazimia kutanguliza mambo yaliyo ya maana zaidi.—Wafilipi 1:10.
-