-
Unaweza ‘Kuifanikisha Njia Yako’ Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2011 | Juni 15
-
-
Kujishughulisha Sana na Kazi ya Kimwili
Neno la Mungu linawatia moyo Wakristo wa kweli wafanye kazi kwa bidii kuwa wafanyakazi na wasimamizi wanaochukua madaraka yao kwa uzito. Mtume Paulo aliandika hivi: “Lolote mnalofanya, lifanyeni kwa nafsi yote kama kwa Yehova, na si kama kwa wanadamu.” (Kol. 3:22, 23) Hata hivyo, ingawa kufanya kazi kwa bidii ni jambo linalostahili pongezi, kuna jambo lingine linalohitajiwa, kuwa na uhusiano mzuri pamoja na Muumba wetu. (Mhu. 12:13) Ikiwa Mkristo atajishughulisha sana na kazi yake ya kimwili, ni rahisi sana kuacha kutanguliza mambo ya kiroho.
Kujishughulisha sana na kazi ya kimwili kunaweza kumfanya Mkristo ahisi kwamba amechoka sana na hivyo hawezi kudumisha usawaziko wake wa kiroho na kuisaidia familia yake. Mfalme Sulemani alisema kwamba “konzi mbili za kazi ngumu” mara nyingi zinaambatana na “kufuatilia upepo.” Ikiwa Mkristo anajishughulisha na kazi ya kimwili kupita kasi, mwishowe atakuwa na mkazo mkali sana kwa muda mrefu. Mtu kama huyo anaweza hata kuwa mtumwa wa kazi na mwishowe anachoka kabisa. Ikiwa ndivyo ilivyo, je, kweli anaweza ‘kufurahi na kuona mema kwa ajili ya kazi yake yote iliyo ngumu’? (Mhu. 3:12, 13; 4:6) Jambo la maana zaidi ni kwamba je, atakuwa na nguvu za kutosha za kimwili na za kihisia za kutimiza madaraka yake katika familia na kushiriki katika utendaji wa kiroho?
Janusz, ambaye anaishi Ulaya Mashariki, alijishughulisha sana na kazi yake ya kutunza mabustani. Anakumbuka hivi: “Watu wa ulimwengu walinipenda kwa sababu nilikuwa mwenye juhudi sana na nilimaliza kila kazi niliyopewa. Lakini hali yangu ya kiroho ilidhoofika, na nikaacha kushiriki katika huduma ya shambani. Muda si muda niliacha kuhudhuria mikutano. Nilikuwa mwenye kiburi sana hivi kwamba nilikataa mashauri ya wazee na nikajitenga na kutaniko.”
-
-
Unaweza ‘Kuifanikisha Njia Yako’ Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2011 | Juni 15
-
-
Kazi ya kimwili: Je, unajishughulisha sana na kazi yako ya kimwili hivi kwamba umeanza kupuuza mambo ya kiroho? Je, unapata wakati wa kutosha wa kuzungumza na familia yako? Je, unaboresha migawo yako ya hotuba katika kutaniko? Je, unashiriki katika mazungumzo yenye kujenga pamoja na wengine? “Mwogope Mungu wa kweli na kushika amri zake,” nawe utapata baraka nyingi za Yehova na ‘utaona mema kwa sababu ya kazi yako ngumu.’—Mhu. 2:24; 12:13.
Janusz, aliyetajwa mwanzoni, hakufanikiwa sana katika biashara yake ya kutunza mabustani; badala yake, alishindwa. Hakupata pesa na alikuwa na madeni makubwa sana, akamgeukia Yehova. Janusz alipanga utendaji wake na sasa anatumika akiwa painia wa kawaida na mzee wa kutaniko. Anasema hivi: “Ninapotosheka na mambo ya msingi na wakati huohuo kujitoa kabisa kiroho, ninapata amani ya akili na utulivu katika moyo.”—Flp. 4:6, 7.
-
-
Unaweza ‘Kuifanikisha Njia Yako’ Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2011 | Juni 15
-
-
KAZI YA KIMWILI
▪ Je, uamuzi wako unakuruhusu ‘ufurahie na kuona mema kwa ajili ya kazi yako yote iliyo ngumu’?
▪ Je, una nguvu za kutosha za kimwili na kihisia za kutimiza madaraka yako katika familia na kushiriki katika utendaji wa kiroho?
▪ Je, unatumia wakati wa kutosha kuzungumza na familia yako?
▪ Je, unajishughulisha sana na kazi hivi kwamba unasukuma kando mambo ya kiroho?
▪ Je, kazi ya kimwili imekuwa na matokeo mabaya kwa migawo yako ya hotuba?
-