-
Mambo Yanayowahatarisha WafanyakaziAmkeni!—2002 | Februari 22
-
-
Misongo Kazini
Mara nyingi, wafanyakazi hulazimishwa kufanya kazi nyingi. Neno karoshi linalomaanisha “kifo kinachosababishwa kwa kufanya kazi kupindukia,” lilitumiwa kwa mara ya kwanza huko Japani wakati familia zilizofiwa zilipodai fidia ya bima. Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa huko miaka mingi iliyopita, asilimia 40 ya watu wanaofanya kazi ofisini huko Japani walihofu kwamba watakufa kwa sababu ya kufanya kazi kupindukia. Wakili mmoja anayehusika na madai ya bima alikadiria kwamba ‘kila mwaka, angalau watu 30,000 huko Japani hufa kwa sababu ya kufanya kazi kupindukia.’
Polisi huko Japani wamedai kwamba matatizo yanayosababishwa na kazi ni kisababishi kikuu cha ongezeko la visa vya kujiua miongoni mwa watu wenye umri wa miaka 50 hadi 59. Kitabu The Violence-Prone Workplace kilisema kuwa mahakama moja ilimhukumu mwajiri fulani kwa kusababisha mwajiriwa wake ajiue kwa sababu ya matatizo mengi kazini.
Gazeti la The Canberra Times la Australia lilisema kwamba ‘Sasa Wamarekani ndio watu wanaofanya kazi kwa saa nyingi zaidi ulimwenguni, na hivyo wamewapita Wajapani.’ Hivyo, habari zenye vichwa kama “Watu Wafa kwa Kufanya Kazi kwa Saa Nyingi” zinaonyesha jinsi wafanyakazi waliochoka, kama vile madereva wa ambulansi, marubani, wajenzi, wafanyakazi wanaotoa huduma za usafiri, na watu wanaofanya kazi usiku wanavyofia kazini.
Makampuni yanapobadili utaratibu na kupunguza idadi ya wafanyakazi ili yaendelee kupata faida, waajiriwa hulazimika kufanya kazi nyingi zaidi. Gazeti la British Medical Journal liliripoti kwamba afya ya waajiriwa huathiriwa wakati idadi ya wafanyakazi inapopunguzwa.
-
-
Mambo Yanayowahatarisha WafanyakaziAmkeni!—2002 | Februari 22
-
-
Profesa Robert L. Veninga wa Chuo Kikuu cha Minnesota, Marekani, anaripoti kwamba “mfadhaiko na madhara yake huwaathiri wafanyakazi katika karibu sehemu zote za ulimwengu.” Alisema kwamba “Ripoti ya Wafanyakazi Ulimwenguni ya 1993, iliyotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Wafanyakazi, ilisema kuwa tatizo kuu ni kwamba mfadhaiko husababishwa na mazingira magumu ya kikazi, yanayobadilika-badilika, na mara nyingi yasiyopendeza.”
-