-
Ona Mema kwa Ajili ya Kazi Yako Ngumu“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
KUTUMIA UTAMBUZI TUNAPOTAFUTA KAZI
14-16. Tunapohitaji kufanya maamuzi kuhusu kazi, ni maswali gani muhimu tunayopaswa kujiuliza?
14 Biblia haina orodha ya kazi za kimwili zinazokubalika na zisizokubalika. Hiyo haimaanishi kwamba tunaweza kukubali kazi yoyote bila kujali mambo yanayohusika. Maandiko yanaweza kutusaidia kuchagua kazi nzuri na iliyo halali ambayo inampendeza Mungu na kuepuka kazi isiyompendeza. (Methali 2:6) Tunapohitaji kufanya maamuzi kuhusu kazi, kuna maswali mawili ya maana tunayopaswa kujiuliza.
15 Je, kazi hiyo inahusisha jambo fulani linaloshutumiwa na Biblia? Neno la Mungu linashutumu waziwazi wizi, udanganyifu, na kutengeneza sanamu. (Kutoka 20:4; Matendo 15:29; Waefeso 4:28; Ufunuo 21:8) Tutakataa kazi yoyote ambayo itatuhusisha katika mambo hayo. Ikiwa tunampenda Yehova, hatuwezi kuchagua kazi inayotuhusisha katika mambo yanayovunja amri za Mungu.—1 Yohana 5:3.
16 Je, kazi hiyo inaweza kufanya tuhusike katika zoea lisilofaa au kuliunga mkono? Fikiria mfano huu. Si vibaya kufanya kazi katika chumba cha kuwapokea wageni. Hata hivyo, namna gani Mkristo akipata kazi kama hiyo katika kliniki ya kutoa mimba? Ni kweli kwamba kazi yake haitamhusisha moja kwa moja katika shughuli za kutoa mimba. Lakini, anapofanya kazi hapo kwa ukawaida, je, hatakuwa akiunga mkono shughuli za kliniki hiyo ya kutoa mimba—zoea lisilopatana na Neno la Mungu? (Kutoka 21:22-24) Kwa kuwa tunampenda Yehova, hatutaki kuhusika katika mazoea yasiyopatana na Maandiko.
17. (a) Ni mambo gani tunayoweza kufikiria kwa makini tunapohitaji kufanya maamuzi kuhusu kazi? (Ona sanduku “Je, Nikubali Kazi Hii?”) (b) Dhamiri yetu inaweza kutusaidia jinsi gani kufanya maamuzi yanayompendeza Mungu?
17 Mambo mengi kuhusu kazi yanaweza kutatuliwa kwa kufikiria kwa makini majibu ya maswali mawili muhimu yaliyo katika fungu la 15 na 16. Pia, kuna mambo mengine tunayopaswa kufikiria kwa makini tunapofanya maamuzi kuhusu kazi.b Hatuwezi kutazamia jamii ya mtumwa mwaminifu iweke sheria kuhusu kila hali inayoweza kutokea. Katika visa kama hivyo, tunahitaji kutumia utambuzi. Kama tulivyojifunza katika Sura ya 2, tunahitaji kuielimisha na kuizoeza dhamiri yetu kwa kujifunza jinsi ya kutumia Neno la Mungu katika maisha yetu ya kila siku. Tukizoeza ‘nguvu zetu za ufahamu kwa kuzitumia,’ dhamiri yetu inaweza kutusaidia kufanya maamuzi yanayompendeza Mungu na kutuwezesha kukaa katika upendo wake.—Waebrania 5:14.
-