-
‘Ufalme Wako Hakika Utakuwa Imara’Mnara wa Mlinzi—2010 | Aprili 1
-
-
Katika mistari ya kwanza ya sura hiyo, tunasoma kwamba Daudi anaona aibu, kwa kuwa, yeye ni mfalme wa kibinadamu tu, lakini anaishi katika jumba maridadi la kifalme, huku sanduku la Mungu likikaa katika hema.a Daudi anasema angependa kumjengea Yehova nyumba, au hekalu zuri. (Mstari wa 2) Lakini si Daudi atakayejenga nyumba hiyo. Kupitia nabii Nathani, Yehova anamwambia Daudi kwamba mwana wake ndiye atakayejenga hekalu hilo.—Mistari 4, 5, 12, 13.
Yehova anapendezwa na tamaa ya Daudi ya moyoni. Kwa hiyo, kupatana na unabii, na pia kwa sababu ya kujitolea kwa Daudi, Mungu anafanya agano naye kwamba atainua mtu fulani katika ukoo wa kifalme wa Daudi ambaye atatawala milele. Nathani anamjulisha Daudi ahadi hii yenye uzito kutoka kwa Mungu: “Nyumba yako na ufalme wako hakika zitakuwa imara mpaka wakati usio na kipimo mbele yako; nacho kiti chako cha ufalme kitafanywa imara mpaka wakati usio na kipimo.” (Mstari wa 16)
-
-
‘Ufalme Wako Hakika Utakuwa Imara’Mnara wa Mlinzi—2010 | Aprili 1
-
-
Pili, masimulizi haya yanatufunza jambo lenye kuchangamsha kumhusu Yehova. Kumbuka kwamba Yehova aliona na kuthamini kile ambacho Daudi alinuia kufanya. Inatia moyo kujua kwamba Yehova anathamini tunapojitolea kwa ajili ya ibada yake. Katika visa fulani, hali tusizoweza kuepuka, kama vile afya inayoendelea kuzorota au uzee, zinaweza kutuzuia kutimiza yale ambayo moyo wetu unatamani kufanya katika kumtumikia Mungu. Ikiwa ndivyo, tunaweza kufarijika kujua kwamba Yehova anaona hata nia ya moyo ambao umejitolea kabisa kwa ajili ya ibada yake.
-