Je, Usemi Wako-Huchoma au Huponya?
NYAKATI hizi ngumu, haishangazi hata kidogo kwamba watu ‘wamevunjika moyo’ na ‘kupondeka roho.’ (Zaburi 34:18) Kwa hiyo, kama alivyosema mtume Paulo, twahitaji kuendelea “[kusema] kwa kuliwaza nafsi zilizoshuka moyo” na ‘kutegemeza walio dhaifu.’ (1 Wathesalonike 5:14) Lakini vipi ikiwa mwanadamu mwenzetu anatukasirisha au kufanya jambo baya sana? Katika kisa kama hicho, huenda tukaona tuna haki ya kumrekebisha vilivyo mtu huyo. Hata hivyo, hadhari yastahili. Shauri, hata liwapo halali, laweza kudhuru likitolewa kwa ukali. Andiko la Mithali 12:18 lataarifu hivi: “Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga.”
Kwa hiyo, tunapoanza kutoa shauri au kushughulikia kutoelewana fulani, ni muhimu kukumbuka sehemu ya pili ya Mithali 12:18: “Ulimi wa mwenye haki ni afya.” Sikuzote jiulize mwenyewe, “Ikiwa mimi ningehitaji kusahihishwa, mimi ningetaka nishughulikiweje?” Wengi wetu huitikia zaidi kitia-moyo kuliko uchambuzi. Kwa hiyo toa pongezi nyingi. Mara nyingi, kufanya hivyo kutamchochea mkosaji kujirekebisha, naye ataelekea kuthamini msaada wowote utolewao.
Ni muhimu kama nini sikuzote kutumia maneno yenye upole! Maneno yenye kuponya yatamfanya msikilizaji ahisi kama alivyohisi mtunga-zaburi ambaye aliandika hivi: “Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; kichwa changu kisikatae.”—Zaburi 141:5.