Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Faraja na Kitia-Moyo Vito Vyenye Pande Nyingi
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Januari 15
    • Kushirikiana na ndugu na dada zetu katika huduma na katika pindi nyingine kwaweza kuwa na matokeo kama hayo. Katika Kiebrania vitenzi kadhaa vinavyomaanisha “kufunganisha pamoja” pia vilikuja kurejezea “nguvu” au “kutia nguvu”—wazo lionekanalo kuonyesha kwamba vitu hupata nguvu zaidi vinapofungwa pamoja. Kanuni hiyo ni kweli katika kutaniko. Sisi hufarijiwa, kutiwa moyo, ndiyo, kutiwa nguvu, kwa kushirikiana pamoja. Na tumefunganishwa pamoja kwa upendo, kifungo chenye nguvu kuliko vyote.—Wakolosai 3:14.

      Nyakati fulani ni uaminifu wa ndugu au dada zetu wa kiroho ambao hututia moyo. (1 Wathesalonike 3:7, 8) Nyakati nyingine ni ule upendo waonyeshao. (Filemoni 7) Na nyakati nyingine ni kule kufanya kazi pamoja, bega kwa bega, tunapozungumza na wengine kuhusu Ufalme wa Mungu. Ukihisi kuwa dhaifu na wahitaji kitia-moyo kwa habari ya huduma, mbona usifanye mipango ya kuhubiri pamoja na mhubiri wa Ufalme mwenye umri mkubwa zaidi au mwenye uzoefu zaidi? Yaelekea utapata faraja nyingi ukifanya hivyo.—Mhubiri 4:9-12; Wafilipi 1:27.

  • Faraja na Kitia-Moyo Vito Vyenye Pande Nyingi
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Januari 15
    • Tumia kikamili fasihi kutoka kwa jamii ya mtumwa mwaminifu. Magazeti, vitabu, na vichapo vingine vya wakati ufaao vyaweza kutusaidia kupata faraja nyakati zinapokuwa ngumu. Kwa upande mwingine, ukiwa katika hali ya kutoa kitia-moyo kwa mtu ambaye ameshuka moyo, tumia habari za Kimaandiko katika majarida haya. Hizo makala huandikwa kwa uangalifu sana, mara nyingi baada ya majuma mengi au miezi mingi ya utafiti, uchunguzi, na sala yenye bidii. Shauri hutegemea Biblia, limejaribiwa na ni la kweli. Wengine wamepata likifaa sana kusoma makala moja au mbili zifaazo pamoja na mtu ambaye ameshuka moyo. Hilo laweza kutokeza faraja na kitia-moyo kingi.

      Ikiwa ungepata vito vyenye thamani, je, ungevificha kwa uchoyo, au ungeshiriki kwa ukarimu hazina hiyo pamoja na wengine? Weka mradi wa kuwa chanzo cha faraja na kitia-moyo kwa ndugu na dada kutanikoni. Ukijenga badala ya kubomoa, kupongeza badala ya kuchambua, kusema “kwa ulimi wa hao wafundishwao” badala ya kusema ‘bila kufikiri kama kuchoma kwa upanga,’ waweza kutokeza tofauti katika maisha za wengine. (Isaya 50:4; Mithali 12:18) Kwa kweli, wewe mwenyewe utaelekea zaidi kuonwa kuwa kito—chanzo cha faraja na kitia-moyo!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki