-
Jinsi Ambavyo Waangalizi Wasafirio Hutumikia Wakiwa Wasimamizi-Nyumba WaaminifuMnara wa Mlinzi—1996 | Novemba 15
-
-
16. Kwa nini inanufaisha sana waangalizi wa mzunguko na wake zao watoapo kitia-moyo?
16 Waangalizi wasafirio hujaribu kuwa wenye kutia moyo. Paulo alipoyazuru makutaniko katika Makedonia, ‘aliyatia moyo kwa maneno mengi.’ (Matendo 20:1, 2, HNWW) Maneno ya kitia-moyo yaweza kuwa yenye msaada sana katika kuwaelekeza vijana na pia wazee kwenye miradi ya kiroho. Kwenye ofisi kubwa moja ya Watch Tower Society, uchunguzi usio rasmi ulifunua kwamba waangalizi wa mzunguko walikuwa wametia moyo karibu asilimia 20 ya wajitoleaji kuanza utumishi wa wakati wote. Kwa kielelezo chake chema akiwa mpiga-mbiu wa Ufalme wa wakati wote, mke wa mwangalizi asafiriye huthibitika pia kuwa chanzo kikubwa cha kitia-moyo.
17. Mwangalizi wa mzunguko mzee-mzee mmoja huhisije juu ya pendeleo lake la kuwatolea wengine msaada?
17 Wazee-wazee na nafsi zilizoshuka moyo wana uhitaji hasa wa kitia-moyo. Mwangalizi wa mzunguko mzee-mzee mmoja aandika hivi: “Sehemu ya kazi yangu itokezayo shangwe ya kindani isiyoelezeka ni pendeleo la kutolea msaada wale wasiotenda na walio wanyonge miongoni mwa kundi la Mungu. Maneno ya Warumi 1:11, 12 (HNWW), yana maana ya pekee kwangu, kwa kuwa mimi hupata kitia-moyo na nguvu nyingi ‘niwagawiapo watu kama hao zawadi ya kiroho na kuwaimarisha.’”
-
-
Jinsi Ambavyo Waangalizi Wasafirio Hutumikia Wakiwa Wasimamizi-Nyumba WaaminifuMnara wa Mlinzi—1996 | Novemba 15
-
-
18. Waangalizi wasafirio wana malengo gani ya Kimaandiko?
18 Waangalizi wasafirio hupendezwa kwa moyo mweupe na waamini wenzao. Wanataka kuyaimarisha makutaniko na kuyajenga kiroho. (Matendo 15:41) Mwangalizi mmoja asafiriye hujitahidi “kutoa kitia-moyo, kuandaa kiburudisho, na kuchochea tamaa ya kutimiza huduma na kuendelea kuishi kulingana na kweli.” (3 Yohana 3) Mwingine hujaribu kuwafanya waamini wenzake wawe thabiti katika imani. (Wakolosai 2:6, 7) Kumbuka kwamba mwangalizi asafiriye ni “mwenzi wa nira halisi,” si bwana-mkubwa juu ya imani ya wengine. (Wafilipi 4:3; 2 Wakorintho 1:24, linganisha NW.) Ziara yake ni pindi ya kupata kitia-moyo na ya utendaji wa ziada, na pia ni fursa kwa baraza la wazee kupitia maendeleo yaliyofanywa na kufikiria miradi ya wakati ujao. Kwa maneno yake na kielelezo chake, watangazaji wa kutaniko, mapainia, watumishi wa huduma, na wazee waweza kutazamia kujengwa na kuchochewa ili kufanya kazi iliyo mbele. (Linganisha 1 Wathesalonike 5:11.) Kwa hiyo, basi, unga mkono kwa moyo wote ziara za mwangalizi wa mzunguko, na kutumia kikamili utumishi unaotolewa na mwangalizi wa wilaya.
-