Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Msimlipe Yeyote Uovu Kwa Uovu”
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 1
    • “Msijilipizie Kisasi Wenyewe”

      15. Andiko la Waroma 12:19 linaonyesha sababu gani ya kutolipiza kisasi?

      15 Paulo anatoa sababu nyingine nzuri ya kutolipiza kisasi; mwenendo huo unaonyesha kwamba tuna sifa ya kiasi. Anasema hivi: “Wapendwa, msijilipizie kisasi wenyewe bali iachieni nafasi ghadhabu; kwa maana imeandikwa: ‘Kisasi ni changu; mimi nitalipa, asema Yehova.’” (Waroma 12:19) Mkristo ambaye anajaribu kulipiza kisasi ana kimbelembele. Anajichukulia daraka ambalo ni la Mungu. (Mathayo 7:1) Kwa kuongezea, anapojichukulia mambo mikononi mwake, anaonyesha kwamba hana imani katika uhakikisho huu wa Yehova: “Mimi nitalipa.” Kinyume cha hilo, Wakristo wa kweli wanasadiki kwamba Yehova “atasababisha haki ifanywe kwa ajili ya watu wake waliochaguliwa.” (Luka 18:7, 8; 2 Wathesalonike 1:6-8) Wanaonyesha sifa ya kiasi kwa kumwachia Mungu daraka la kulipiza uovu.—Yeremia 30:23, 24; Waroma 1:18.

      16, 17. (a) Ni nini maana ya ‘kukusanya makaa yenye moto’ juu ya kichwa cha mtu? (b) Je, wewe binafsi umeona fadhili ikiondoa chuki katika moyo wa mtu ambaye si mwamini? Ikiwa umeona, toa mfano.

      16 Inaelekea kwamba kumlipiza adui kisasi kunaweza kufanya moyo wake uwe mgumu, lakini kumtendea kwa fadhili kunaweza kuondoa chuki yake. Kwa nini? Angalia maneno ambayo Paulo anawaambia Wakristo huko Roma. Anasema hivi: “Ikiwa adui yako ana njaa, mlishe; ikiwa ana kiu, mpe kitu anywe; kwa maana kwa kufanya hivyo utakusanya makaa yenye moto juu ya kichwa chake.” (Waroma 12:20; Methali 25:21, 22) Hilo linamaanisha nini?

      17 ‘Kukusanya makaa yenye moto juu ya kichwa chake’ ni usemi wa mfano ambao unatokana na njia iliyotumiwa kuyeyusha vyuma katika nyakati za Biblia. Mawe yenye chuma yalitiwa katika tanuru ya moto, na makaa yakawekwa juu na pia chini ya mawe hayo. Makaa yenye moto yaliyokusanywa juu ya vyuma yaliongeza joto ambalo liliyeyusha vyuma vigumu na kuvitenganisha na uchafu uliokuwa ndani ya mawe hayo. Vivyo hivyo, tunapomtendea mpinzani kwa fadhili, tunaweza “kuyeyusha” ugumu wake na kumfanya aonyeshe sifa zake nzuri. (2 Wafalme 6:14-23) Kwa kweli, washiriki wengi wa kutaniko la Kikristo walivutiwa na ibada ya kweli kwa sababu ya kutendewa kwa fadhili na watumishi wa Yehova.

  • “Msimlipe Yeyote Uovu Kwa Uovu”
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 1
    • Tatu, tunaonyesha sifa ya kiasi kwa kutolipa uovu kwa uovu. Kujilipizia kisasi ni kuwa na kimbelembele, kwa kuwa Yehova anasema: “Kisasi ni changu.” Neno la Mungu linatuonya hivi pia: “Je, kimbelembele kimekuja? Basi aibu itakuja; lakini wenye kiasi wana hekima.” (Methali 11:2) Tunaonyesha sifa ya kiasi tunapomwachia Mungu daraka la kulipiza uovu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki