Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Akila na Prisila—Wenzi Walio Kielelezo Chema
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 15
    • Urafiki wao na Paulo ulikuwa wa karibu sana hivi kwamba Akila na Prisila waliondoka Korintho pamoja naye katika masika ya mwaka wa 52 W.K., wakiandamana naye hata kufikia Efeso. (Matendo 18:18-21) Walikaa katika jiji hilo na kuwekea msingi ziara ambayo ingefuata ya huyo mtume. Hapo ndipo walimu hao stadi wa habari njema walipomchukua Apolo mwenye ufasaha “kwao” na kuwa na shangwe ya kumsaidia aelewe “njia ya Bwana kwa usahihi zaidi.” (Matendo 18:24-26) Paulo alipozuru Efeso tena wakati wa safari yake ya tatu ya umishonari, wakati fulani karibu na kipupwe cha mwaka wa 52/53 W.K., shamba lililokuwa limelimwa na wenzi hao wenye nishati lilikuwa tayari kwa mavuno. Kwa miaka mitatu hivi, Paulo alihubiri na kufundisha huko juu ya “Njia ile,” huku kutaniko la Efeso likifanya mikutano nyumbani mwa Akila.—Matendo 19:1-20, 26; 20:31; 1 Wakorintho 16:8, 19.

  • Akila na Prisila—Wenzi Walio Kielelezo Chema
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 15
    • Labda Paulo aliishi pia na Akila na Prisila alipokuwa Efeso. Je, alikuwa akikaa nao wakati wa ile vurugu ya wafua-fedha? Kulingana na simulizi kwenye Matendo 19:23-31, wale wasanii waliofanyiza vihekalu walipoasi dhidi ya kuhubiriwa kwa habari njema, hao ndugu walilazimika kumzuia Paulo asijihatarishe kwa kwenda mbele ya kikundi cha wafanya-ghasia. Waelezaji fulani wa Biblia wametoa nadharia ya kwamba huenda ikawa ni katika wakati huo barabara wa hatari ambapo Paulo ‘alikata tamaa ya kuishi’ na kwamba Akila na Prisila waliingilia katika njia fulani, ‘wakiwa tayari hata kukatwa kichwa’ kwa ajili yake.—2 Wakorintho 1:8; Warumi 16:3, 4.

      “Kishindo kile kilipokoma,” Paulo aliondoka hilo jiji kwa hekima. (Matendo 20:1) Bila shaka Akila na Prisila walikabili pia upinzani na dhihaka. Je, hilo liliwafanya wavunjike moyo? Kinyume na hivyo, Akila na Prisila waliendelea kwa moyo mkuu katika juhudi zao za Kikristo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki