-
Aliwatetea Watu wa MunguMnara wa Mlinzi—2011 | Oktoba 1
-
-
Alipata Kibali “Machoni pa Kila Mtu Aliyemwona”
Maisha ya Esta yalibadilika na kuwa tofauti kabisa. Alikuwa kati ya “wanawake wengi vijana” waliokuwa wamekusanywa kutoka maeneo mbalimbali ya Milki ya Uajemi. Lazima tamaduni, lugha, na mitazamo yao ilitofautiana kabisa. Chini ya usimamizi wa ofisa anayeitwa Hegai, wanawake hao vijana wangerembeshwa sana katika programu ya mwaka mmoja iliyotia ndani kukandwa kwa mafuta yenye marashi. (Esta 2:8, 12) Huenda hali hiyo ilifanya wasichana hao wafikirie sana urembo wao, wawe na kiburi, na kushindana. Esta aliathiriwa jinsi gani?
Bila shaka, Mordekai alijali sana hali ya Esta. Tunasoma kwamba siku baada ya siku, alienda karibu wa nyumba ya wanawake ili apate kujua hali ya Esta. (Esta 2:11) Habari chache alizopata, labda kutoka kwa wafanyakazi walioshirikiana naye, lazima zilimfurahisha sana. Kwa nini?
Hegai alivutiwa sana na mwenendo wa Esta hivi kwamba alimtendea kwa fadhili sana na kumpa vijakazi saba na mahali bora zaidi katika nyumba ya wanawake. Simulizi hilo hata linasema hivi: “Wakati huo wote Esta alikuwa akizidi kupata kibali machoni pa kila mtu aliyemwona.” (Esta 2:9, 15) Je, urembo peke yake ndio uliofanya kila mtu avutiwe sana naye? Hapana, Esta alikuwa na sifa nyingine nzuri.
-
-
Aliwatetea Watu wa MunguMnara wa Mlinzi—2011 | Oktoba 1
-
-
Wakati ulipofika wa Esta kupelekwa kwa mfalme, alipewa nafasi ya kuchagua vitu ambavyo alifikiri angehitaji, labda vitu ambavyo angetumia kujirembesha zaidi. Hata hivyo, kwa kufuata shauri la Hegai, Esta alikuwa na kiasi na hakuomba kitu chochote zaidi ya vitu alivyopewa. (Esta 2:15) Yaelekea alijua kuwa urembo pekee haungeweza kufurahisha moyo wa mfalme; kiasi na unyenyekevu zilikuwa sifa muhimu mbele ya mfalme. Je, ni kweli?
Simulizi linajibu hivi: “Mfalme akampenda Esta kuliko wale wanawake wengine wote, hata akapata kibali na fadhili zenye upendo kuliko wale mabikira wengine wote. Ndipo mfalme akamvika taji la kifalme juu ya kichwa chake na kumfanya kuwa malkia badala ya Vashti.” (Esta 2:17)
-