-
Ole wa Pili—Majeshi ya Wapanda-FarasiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
ikisema kwa malaika wa sita, ambaye alikuwa na tarumbeta: ‘Fungua malaika wanne ambao wamefungwa kwenye mto mkubwa Eufrati.’” (Ufunuo 9:13, 14, NW)
-
-
Ole wa Pili—Majeshi ya Wapanda-FarasiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
3. Ni jinsi gani malaika wanne walikuwa “wamefungwa kwenye mto mkubwa Eufrati”?
3 Ni jinsi gani malaika hao walikuwa “wamefungwa kwenye mto mkubwa Eufrati”? Katika nyakati za kale mto Eufrati ulikuwa ndio mpaka wa kaskazini-mashariki wa lile bara ambalo Yehova alikuwa amemwahidi Abrahamu. (Mwanzo 15:18; Kumbukumbu 11:24) Kwa wazi, hao “malaika” walikuwa wamezuiliwa mpakani mwa bara lao walilopewa na Mungu, au milki ya kidunia ya utendaji, wakizuiwa wasiingie kabisa ndani ya utumishi ambao Yehova alikuwa amewatayarishia. Pia Eufrati ulikuwa umeshirikishwa sana na lile jiji la Babuloni, na baada ya anguko la Yerusalemu katika 607 K.W.K., Waisraeli wa mnofu walitumia miaka 70 huko katika utekwa, ‘wakiwa wamefungwa kwenye mto mkubwa Eufrati.’ (Zaburi 137:1) Mwaka wa 1919 uliwapata Waisraeli wa kiroho wakiwa wamefungwa katika kizuizi kama hicho, wakiwa wamehuzunika na wakiomba Yehova wapate mwongozo.
-