-
Isikie Sauti Inayotoka NdaniMnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 15
-
-
Mwelekeo wa kuwasaidia wengine, hata kwa hasara ya kibinafsi, umeenea sana leo hivi kwamba watu fulani wanauita mwelekeo huo “ubinadamu.”
4 Mwelekeo huo wa kuwa tayari kuwasaidia wengine hata kwa hasara ya kibinafsi unaonekana katika jamii na tamaduni zote, na unapinga dai la kwamba mwanadamu anaongozwa na kanuni ya kwamba unapaswa kutimiza kwanza mahitaji yako mwenyewe, yaani, “viumbe bora ndio wanaosalimika.” Francis S. Collins, mtaalamu wa chembe za urithi ambaye aliongoza jitihada za serikali ya Marekani za kuelewa chembe za urithi za mwanadamu (DNA au ADN), alisema hivi: “Kuwajali wengine bila ubinafsi ni tatizo kubwa kwa mwana-mageuzi. . . . Sifa hiyo haipatani na wazo la kwamba tunachochewa na chembe za urithi zenye ubinafsi.” Pia, alisema: “Watu fulani wanajitolea wenyewe kuwasaidia wale ambao si wa jamii yao na ambao hawana uhusiano wowote nao. . . . Inaonekana kwamba sifa ya kuwajali wengine haiwezi kufafanuliwa na nadharia ya Darwin.”
-
-
Isikie Sauti Inayotoka NdaniMnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 15
-
-
a Vivyo hivyo, Owen Gingerich, profesa wa utafiti wa elimu ya nyota kwenye Chuo Kikuu cha Harvard, aliandika hivi: “Kwa kweli, huenda kuwajali wengine kukatokeza swali ambalo . . . haliwezi kujibiwa kisayansi kutokana na uchunguzi wa wanyama. Huenda ikawa kwamba jibu linalosadikisha zaidi linatokana na chanzo kingine na linahusiana na sifa za ubinadamu ambazo tumepewa na Mungu, zinazotia ndani dhamiri.”
-