-
Kwa Nini Wanasayansi Fulani Humwamini Mungu?Amkeni!—2004 | Juni 22
-
-
Donald E. Chittick, mwanakemia aliyepata shahada katika Chuo Kikuu cha Jimbo la Oregon, anasema hivi: “Kuchunguza rekodi ya mabaki ya viumbe vya kale kwa makini humfanya mtu afikie mkataa wa kwamba wanyama walizaa kulingana na aina zao, kama vile kitabu cha Mwanzo kinavyosema. Hawakugeuka na kuwa aina nyingine. Uthibitisho uliopo sasa, kama ilivyokuwa wakati wa Darwin, unapatana na rekodi ya kitabu cha Mwanzo ya kwamba viumbe viliumbwa moja kwa moja. Mimea na wanyama wanaendelea kuzaa kulingana na aina zao. Kwa kweli, kuna tofauti kubwa sana kati ya uchunguzi wa mabaki ya viumbe vya kale na nadharia ya Darwin, hivi kwamba wanasayansi fulani wameanza kuamini kwamba mabaki ya viumbe vilivyokuwa vikigeuka hayatapata kuonekana.”
-
-
Kwa Nini Wanasayansi Fulani Humwamini Mungu?Amkeni!—2004 | Juni 22
-
-
Hivyo, baada ya kufanya utafiti na uchunguzi wa kisayansi wenye mafanikio kwa muda mrefu, mtaalamu wa anga Allan Sandage alisema: “Uchunguzi wangu wa kisayansi ndio ulionichochea kufikia mkataa wa kwamba ulimwengu ni tata sana hivi kwamba hauwezi kuelezeka kisayansi. Ninaweza kuelewa chanzo cha vitu vilivyopo kupitia tu chanzo fulani kisicho cha kibinadamu.”
-
-
Unaweza Kupata Wapi Majibu?Amkeni!—2004 | Juni 22
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 9]
Maoni ya wanasayansi wenyewe
Wanasayansi wengi wanatangaza waziwazi imani yao katika Muumba. Ingawa baadhi yao wana maoni yasiyo wazi kabisa kumhusu Mungu, bado wanakubali kwamba uthibitisho unaonyesha kuna Mbuni mwenye akili. Hebu fikiria maelezo yanayofuata:
“Nikiwa mwanasayansi, mimi huutazama ulimwengu, na kuona utaratibu wenye utata sana hivi kwamba ninachochewa kukata kauli kwamba utaratibu huo tata ulibuniwa kwa akili.”—ANDREW MCINTOSH, MWANAHISABATI, HUKO WALES, UINGEREZA
“Utata wa mambo ya asili huonyesha wazi kwamba kuna Muumba. Mifumo yote ya kibiolojia na kifizikia, inapoeleweka, inaonyesha utata wa ajabu.”—JOHN K. G. KRAMER, MTAALAMU WA BIOKEMIA, HUKO KANADA
“Ni wazi kwamba kuna utaratibu katika viumbe ulimwenguni. Vilitokana na Nguvu kuu zaidi ambazo mimi mwenyewe ninaziita Mungu. Hapa ndipo imani inapopatana na kweli ya kisayansi. Badala ya kuipinga sayansi, imani inaikamilisha, ikitoa maelezo sahili kuhusu ulimwengu wetu.”—JEAN DORST, MWANABIOLOJIA, HUKO UFARANSA
“Siwezi kuwazia kwamba ulimwengu na uhai wa wanadamu haukutokana na mtu fulani mwenye akili, au chanzo kingine cha kiroho chenye hisia, kisichohusisha mata na sheria zake.”—ANDREY DMITRIYEVICH SAKHAROV, MWANAFIZIKIA WA NYUKLIA, HUKO URUSI
“Kila mnyama amebuniwa kwa njia ya pekee ili aweze kuishi katika mazingira yake, nami sina budi kusema kwamba utata wa ubuni huo umetokana na Muumba, wala si nguvu za mageuzi zisizo na mpango.”—BOB HOSKEN, MTAALAMU WA BIOKEMIA, HUKO AUSTRALIA
-