Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yesu Aja na Kitia-Moyo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Tazama! Yeye anakuja pamoja na mawingu, na kila jicho litaona yeye, na wale ambao walidunga yeye; na makabila yote ya dunia yatajipigapiga kwa kihoro kwa sababu yake yeye. Ndiyo, Ameni.” (Ufunuo 1:7, NW)

  • Yesu Aja na Kitia-Moyo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Jinsi gani, basi, “kila jicho litaona yeye”? Haitupasi kutaraji kwamba adui za Yesu wangemwona kwa jicho halisi, kwa kuwa mtume Paulo alisema, baada ya Yesu kupaa mbinguni, kwamba Yesu sasa “amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa,” na “hakuna mwanadamu aliyemwona, wala aweza kumwona.” (1 Timotheo 6:16) Kwa wazi, Yohana alimaanisha ‘kuona’ katika maana ya ‘kufahamu’ kama vile sisi tunavyoweza kuona, au kufahamu, sifa za Mungu zisizoonekana kwa njia ya uumbaji wake. (Warumi 1:20) Yesu “anakuja pamoja na mawingu” katika maana ya kwamba yeye atakuwa asiyeonekana kwa jicho tupu kama vile jua linavyokuwa likiwa nyuma ya mawingu. Hata wakati jua linapofichwa na mawingu wakati wa mchana, sisi tunajua lipo kwa sababu ya nuru ya mchana inayotuzunguka. Vivyo hivyo, ingawa Bwana Yesu haonekani, yeye atafunuliwa kama ‘moto wenye kuwaka mwali, aletapo kisasi juu ya wale ambao hawatii habari njema kuhusu yeye.’ Hawa pia watalazimishwa ‘kuona yeye.’—1 Wathesalonike 1:6-8, NW; 2:8.

      8. (a) Ni nani waliokuwa “wale ambao walidunga yeye” katika 33 W. K., na ni nani hao leo? (b) Kwa kuwa Yesu hayupo hapa duniani tena, watu wanawezaje ‘kudunga yeye’?

      8 Yesu ‘ataonwa’ pia na “wale ambao walidunga yeye.” Hao wanaweza kuwa akina nani? Wakati Yesu alipouawa katika 33 W.K., askari wa Roma walidunga yeye kihalisi. Hatia ya uuaji huo wa kukusudia ilishirikiwa pia na Wayahudi, kwa kuwa Petro aliambia baadhi ya hao hivi kwenye Pentekoste: “Mungu alifanya yeye kuwa Bwana na pia Kristo, huyu Yesu ambaye nyinyi mlitundika juu ya mti.” (Matendo 2:5-11, 36, NW; linga Zekaria 12:10; Yohana 19:37.) Waroma na Wayahudi hao sasa wamekuwa wafu kwa karibu miaka 2,000. Kwa hiyo wale ‘waliodunga yeye’ leo lazima wawakilishe mataifa na vikundi vya watu wanaoonyesha mwelekeo ule ule wenye chuki ulioonyeshwa wakati Yesu alipotundikwa juu ya mti. Yesu hayupo tena hapa duniani. Lakini wakati wapinzani wanaponyanyasa Mashahidi wa Yehova, ambao hutoa ushuhuda juu ya Yesu, ama kwa kutenda ama kwa kutotenda wanapokubali watendwe hivyo, ni kama tu wapinzani hao walikuwa ‘wakidunga’ Yesu mwenyewe.—Mathayo 25:33, 41-46.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki