Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Endeleeni Kutembea Katika Upendo”
    Mkaribie Yehova
    • Mkristo mwenye umri mkubwa anaonyesha kwamba anamtumaini mwamini mwenzake kijana.

      Upendo hutuchochea tuwaamini ndugu zetu

      12. Mtume Paulo alionyeshaje aliamini kwamba Filemoni angetenda ifaavyo, na mfano wa Paulo unatufunza nini?

      12 ‘Upendo huamini mambo yote.’ Tafsiri ya Moffat inasema kwamba upendo “sikuzote hujitahidi kuamini mambo mazuri.” Hatuwashuku isivyofaa waamini wenzetu na kutilia shaka kila jambo wanalofanya. Upendo unatusaidia “kuamini mambo mazuri” kuhusu ndugu zetu na kuwatumaini.a Fikiria mfano unaotajwa katika barua ya Paulo kwa Filemoni. Paulo alimwandikia Filemoni ili kumtia moyo amkaribishe kwa fadhili Onesimo yule mtumwa mtoro, ambaye sasa alikuwa Mkristo. Paulo alimsihi Filemoni kwa upendo badala ya kujaribu kumlazimisha. Aliamini kwamba Filemoni angetenda ifaavyo, kwa kusema: “Nikiitibari ukubalifu wako wa kufuata agizo, ninakuandikia wewe, nikijua utafanya hata zaidi ya mambo nisemayo.” (Mstari wa 21) Upendo unapotuchochea kuwaamini ndugu zetu, tunawatia moyo kufanya yote wawezayo.

  • “Endeleeni Kutembea Katika Upendo”
    Mkaribie Yehova
    • a Bila shaka, upendo wa Kikristo si wa kijinga. Biblia inatuhimiza hivi: “Mfulize kuangalia wale wasababishao migawanyiko na sababu za kukwaza . . . , na mwaepuke.”—Waroma 16:17.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki