Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unaweza Kuwa na Imani ya Kweli
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Oktoba 1
    • Unaweza Kuwa na Imani ya Kweli

      Wakati Sarah Jayne alipokuwa na umri wa miaka 19, aligundua kwamba ana kansa ya ovari. Baada ya kufanyiwa upasuaji, alipata nafuu na akawa na matumaini mema ya wakati ujao. Alikuwa na matumaini mema sana hivi kwamba alipofika umri wa miaka 20, alichumbiwa na akaanza kufanya mipango ya arusi. Mwaka huohuo, alishikwa tena na kansa hiyo, na akagundua kwamba angekufa baada ya majuma machache tu. Sarah Jayne alikufa mnamo Juni 2000, kabla tu hajafikisha umri wa miaka 21.

      WAGENI walioenda kumwona Sarah Jayne hospitalini walivutiwa sana na uhakika aliokuwa nao kuhusu wakati ujao, pamoja na imani yake thabiti katika Mungu na katika Neno lake, Biblia. Licha ya msiba aliokuwa akikabili, alikuwa na tumaini hakika la ufufuo—kwamba angewaona tena marafiki wake wote. (Yohana 5:28, 29) Alisema, “nitawaona nyinyi nyote katika ulimwengu mpya wa Mungu.”

  • Unaweza Kuwa na Imani ya Kweli
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Oktoba 1
    • Sarah Jayne alipata kufahamu kwamba Biblia ni Neno la Mungu lililopuliziwa. (1 Wathesalonike 2:13; 2 Petro 1:19-21) Jinsi gani? Si kwa sababu wazazi wake walimwambia tu aamini hivyo, bali kwa sababu alichunguza kwa unyofu uthibitisho wote unaoonyesha kwamba Biblia ni ufunuo wa kipekee kutoka kwa Mungu. (Waroma 12:2) Kwa mfano, aliona jinsi Biblia ilivyo na uvutano wenye nguvu katika maisha ya wale wanaotii kanuni zake. Pia kwa msaada wa vichapo kama vile Biblia—Neno la Mungu au la Mwanadamu?,b alichunguza kwa makini uthibitisho mwingi sana unaoonyesha kwamba Biblia imepuliziwa na Mungu.

  • Unaweza Kuwa na Imani ya Kweli
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Oktoba 1
    • Sarah Jayne alikuwa ameshawishiwa jinsi hiyo. Kama Waberoya wa karne ya kwanza, ‘alilipokea neno kutoka kwa wazazi wake kwa hamu ya akili iliyo kubwa zaidi sana.’ Akiwa mtoto mdogo, bila shaka alitumaini mambo aliyoambiwa na wazazi wake. Baadaye, alipoendelea kukua, hakukubali tu kila jambo alilofundishwa. ‘Aliyachunguza Maandiko kwa uangalifu kila siku juu ya kama mambo hayo yalikuwa hivyo.’—Matendo 17:11.

  • Unaweza Kuwa na Imani ya Kweli
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Oktoba 1
    • Sarah Jayne aliona ukweli wa jambo hilo, na sikuzote aliwatia moyo wale waliomtembelea hospitalini wasitawishe imani yao. Alikuwa akisema, “Fanya ukweli uwe njia yako ya maisha. Jifunze Neno la Mungu. Kaa karibu na tengenezo la Mungu. Sali daima. Uwe mwenye bidii katika utumishi wa Yehova.”—Yakobo 2:17, 26.

      Alipoona imani ya Sarah Jayne katika Mungu na katika ufufuo, muuguzi mmoja alisema hivi: “Ni kweli kwamba unaamini mambo hayo.” Alipoulizwa ni nini kilichomsaidia kuwa na mtazamo mzuri namna hiyo licha ya majaribu yaliyompata, alijibu: “Ni kuwa na imani katika Yehova. Yeye ni rafiki yangu wa kweli, nami nampenda sana.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki