Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • New Zealand

      Dada wawili walienda kwenye ofisi za shirika la serikali la mfuko wa hazina ya familia nao wakafanya mipango ya kuja kumwona mkurugenzi wa shirika hilo. Ili kujiandaa kwa ajili ya ziara hiyo, walitayarisha “kifurushi cha familia,” kilichokuwa na habari za pekee ambazo zingemvutia mkurugenzi huyo katika kazi yake ya kushughulika na familia. Walitia ndani vitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia na Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi pamoja na toleo la Amkeni! la Agosti 2007, lililokuwa na makala “Hatua Saba za Kuwa Mzazi Bora” na pia Amkeni! la Oktoba (Mwezi wa 10) 2007 lililokuwa na makala “Walinde Watoto Wako!”

      Walipoenda kumwona mkurugenzi wa shirika hilo, dada zetu walimweleza kuhusu kazi yetu ya kujitolea na kumwambia kwamba tunapendezwa sana kusaidia familia, hasa kwa njia ya kiroho. Walimwonyesha vitabu na magazeti yaliyokuwa katika kifurushi walichotayarisha. Mkurugenzi huyo alisikiliza, akapokea vitabu na magazeti hayo, na kusema kwamba angependa wale wafanyakazi wengine 35 wafaidike pia na ujumbe huo. Aliongeza kwamba makala za Amkeni! zitanufaisha familia zote 503 zilizo katika rekodi zake. Dada hao walikusanya nakala 557 za gazeti hilo la Amkeni! Majuma wawili baadaye, walipokea simu kwamba magazeti yote hayo yalikuwa yametumwa kwa familia hizo.

  • Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 63]

      Kutayarisha “kifurushi cha familia”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki