-
Naweza Kuishije Nikiwa na Huzuni Yangu?Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
-
-
“NILIHISI kusongwa sana nizuie hisia zangu,” aeleza Mike alipokumbuka kifo cha baba yake. Kwa Mike, kuzuia huzuni yake lilikuwa jambo la kiume kufanya. Hata hivyo baadaye aling’amua kwamba alikuwa amekosea. Kwa hiyo rafikiye Mike alipofiwa na babu yake, Mike alijua jambo la kufanya. Yeye asema hivi: “Miaka michache iliyopita, ningalimpigapiga begani na kusema ‘Uwe mwanamume.’ Sasa niligusa mkono wake na kusema, ‘Hisi vile utakavyo kuhisi. Hilo litakusaidia ushughulike vya kufaa na hali hii. Ikiwa wataka niende, nitaenda. Ikiwa wataka nikae, nitakaa. Lakini usiogope kuhisi.’”
-
-
Naweza Kuishije Nikiwa na Huzuni Yangu?Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
-
-
Kwa hiyo Mike na pia MaryAnne wanapendekeza hivi: Jiruhusu uhuzunike! Nao wasema kweli. Kwa nini? Kwa sababu kuhuzunika ni ondoleo la kihisiamoyo linalohitajika. Kuondosha hisia zako kwaweza kutuliza ule msongo unaokabili. Wonyesho wa asili wa hisiamoyo, pamoja na uelewevu na habari sahihi, unakuruhusu uzionyeshe hisia zako ifaavyo.
-
-
Naweza Kuishije Nikiwa na Huzuni Yangu?Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
-
-
Mwanamke mmoja mchanga aeleza jinsi rafiki wa karibu alivyomsaidia ashughulike vya kufaa na hali wakati mama yake alipokufa. Yeye akumbuka hivi: “Sikuzote rafiki yangu alikuwapo kwa ajili yangu. Alilia pamoja nami. Aliongea nami. Niliweza tu kuonyesha hisiamoyo zangu waziwazi sana, na hilo lilikuwa jambo la maana kwangu. Sikuhitaji kuaibika kwa sababu ya kulia.” (Ona Warumi 12:15.) Wewe pia hupaswi kuaibika kwa sababu ya machozi yako. Kama vile tumeona, Biblia imejaa vielelezo vya wanaume na wanawake wa imani—kutia na Yesu Kristo—waliolia machozi ya huzuni waziwazi bila kuonekana kuwa na aibu.—Mwanzo 50:3; 2 Samweli 1:11, 12; Yohana 11:33, 35.
Huenda ukaona kwamba kwa wakati fulani hisiamoyo zako zitatokea bila kutazamiwa. Huenda machozi yakatiririka bila ya wewe kujua kimbele. Mjane mmoja aliona kwamba kununua vitu kwenye duka kubwa (jambo alilokuwa amefanya mara nyingi pamoja na mume wake) kuliweza kumfanya alie, hasa wakati, kwa sababu ya kuzoea, alipofikia ili achukue vyakula vilivyopendwa sana na mume wake. Jionyeshe saburi. Na usihisi kwamba ni lazima uyazuie machozi yasitoke. Kumbuka, hiyo ni sehemu ya asili na ya lazima ya kuhuzunika.
-
-
Naweza Kuishije Nikiwa na Huzuni Yangu?Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
-
-
‘Lakini kuna mambo mengi sana ambayo laiti ningalisema au kufanya,’ huenda ukasema. Ni kweli, lakini ni nani kati yetu awezaye kusema kwamba sisi tumekuwa baba, mama, au mtoto mkamilifu? Biblia hutukumbusha hivi: “Sisi sote hujikwaa mara nyingi. Ikiwa yeyote hajikwai katika neno, huyu ni mtu mkamilifu.” (Yakobo 3:2; Warumi 5:12, NW) Kwa hiyo kubali uhakika wa kwamba wewe si mkamilifu. Kuendelea kufikiri-fikiri ati “laiti tu ningalifanya hivi au vile” hakutabadili chochote, lakini huenda kwaweza kukawiza kupata kwako nafuu.
Ikiwa una sababu nzuri za kuamini kwamba hatia yako ni halisi, isiyowaziwa tu, basi fikiria lile jambo la maana zaidi ya yote katika kutuliza hisia ya kuwa na hatia—msamaha wa Mungu. Biblia hututia moyo hivi: “BWANA, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama? Lakini kwako kuna msamaha.” (Zaburi 130:3, 4) Huwezi kurudia wakati uliopita na kubadili chochote. Lakini, waweza kumwomba Mungu msamaha kwa makosa ya wakati uliopita. Kisha nini? Ikiwa Mungu anaahidi kufuta kabisa makosa yako, je, wewe hupaswi pia kujisamehe?—Mithali 28:13; 1 Yohana 1:9.
-