Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tamaa ya Kusafiri Salama kwa Ndege
    Amkeni!—2002 | Desemba 8
    • Kusafiri Tena kwa Ndege

      Baada ya kukataa kusafiri kwa ndege kwa miezi minne, Alex aliamua kupambana na woga wake. Ijapokuwa polisi na wanajeshi walikuwapo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Logan huko Boston, yeye hakubabaika. Hakuona ubaya wowote kupanga foleni ndefu wala mizigo yake kukaguliwa.

      Alex aliona hatua hizo kuwa dalili zenye kutia moyo kwani anatamani sana usafiri wa ndege uwe salama. Bado yeye ana wasiwasi kidogo. Hata hivyo, anapopakia mfuko wake uliokaguliwa ndani ya ndege, anasema hivi: “Sasa ninahisi afadhali zaidi.”

  • Kuhangaikia Usalama
    Amkeni!—2002 | Desemba 8
    • Kuhangaikia Usalama

      KUSAFIRI kwa ndege kilometa 11 juu ya dunia kwaweza kuwaogopesha watu fulani. Huenda likaonekana kuwa jambo lisilopatana na sheria za asili. Kwa kuwa sasa usalama umeimarishwa na usafiri wa ndege unategemeka zaidi, hatari zinazoweza kutokea kwa kusafiri haraka ndani ya ndege zimepungua. Hata hivyo, misiba ya ndege hutukia mara mojamoja.

      Kukabiliana na Woga

      Ingawa msiba unaweza kutokea, tangu zama za kale, mwanadamu ameonyesha tamaa yake ya kusafiri hewani. Miaka elfu moja kabla ya Kristo, Mfalme Daudi aliandika hivi: “Laiti ningekuwa na mabawa kama njiwa! Ningeruka mbali.” (Zaburi 55:6, Biblia Habari Njema) Kama ilivyotajwa tayari, tekinolojia ya kisasa imefanya usafiri wa ndege uwe mojawapo ya njia salama zaidi za kusafiri. Lakini usafiri huo haukosi dosari. Hakuna kitu ulimwenguni kilicho salama kabisa wala kinachoweza kujulikana kimbele kwa ukamili.

      Ni muhimu kukumbuka jambo hilo iwapo tunakuwa na wasiwasi wakati mtu mwingine anapoendesha mambo. Watu wengine wanaweza kufikiri hivi, ‘Mimi mwenyewe nikiendesha shughuli fulani, wasiwasi wangu hupungua.’ Watu kama hao wanaweza kusumbuka sana wanapojipata mahali ambapo hawawezi kufanya lolote au hawana uhuru wa kudhibiti mambo. Usafiri wa ndege ni mojawapo ya hali hizo.

      Licha ya jitihada za kuimarisha usalama katika usafiri wa ndege, mtu yeyote hapaswi kuchukua mambo kimchezo. Wote wanaohusika katika usafiri wa ndege wanaweza kushirikiana kupunguza visababishi vya hatari. Na bado wenye mamlaka hutoa maonyo kuhusu hatari zilizopo. Mithali moja yenye hekima katika Biblia inasema: “Mtu mwenye busara huona hatari iliyo mbele mapema na kutahadhari.” (Mithali 22:3, New Living Translation) Ni jambo la hekima kutambua kwamba hatari fulani yaweza kutokea katika shughuli yoyote ile. Kumbuka kwamba mtu anaposafiri kwa ndege anapaswa kuchukua tahadhari zilezile za kujilinda ambazo zinahitajika katika hali nyinginezo.

      Watu ambao husafiri kwa ndege mara nyingi wanaweza kujua vizuri zaidi jinsi ya kushughulika na hali hizo ngumu. Hiyo ni kwa sababu wamezoea ndege na viwanja vya ndege kuliko abiria wengine. Wewe pia unaweza kuzoea hali hizo na kustarehe kama wao kwa kufuata hatua sahili zinazoonyeshwa kwenye masanduku yaliyo katika makala hii.

  • Kuhangaikia Usalama
    Amkeni!—2002 | Desemba 8
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 12]

      KUWATULIZA WATU WA FAMILIA YAKO

      Madokezo yafuatayo yanaonyesha jinsi unavyoweza kuwasaidia watu wa familia yako wasiwe na wasiwasi unaposafiri. Yametolewa kwenye kituo cha Internet cha United Behavioral Health

      Zungumza na watu wa familia yako. Kabla ya kwenda safarini, tumia muda fulani pamoja na wapendwa wako ili mzungumzie usalama wako na vilevile usalama wao. Eleza hatua mpya ambazo zimechukuliwa kuimarisha usalama na jinsi zinavyochangia usalama wako unaposafiri.

      Acha waeleze mahangaiko yao. Acha watu wa familia yako waeleze wasiwasi wao. Wanakupenda na wanataka tu uwe salama. Sikiliza kwa makini bila kuwachambua, na uchukue mahangaiko yao kwa uzito.

      Wape uhakikisho wa kweli. Zungumzia jinsi ambavyo mashirika mbalimbali yanajaribu kuzuia mashambulizi mengine ya magaidi. Hiyo inatia ndani hatua zaidi za kuimarisha usalama kwenye viwanja vya ndege na ndani ya ndege. Uwezekano wa msiba kutokea unaposafiri kwa ndege ni mdogo sana.

      Endelea kuwasiliana nao. Waahidi kuwa utawapigia simu utakapofika. Endelea kupiga simu nyumbani kwa ukawaida kwa muda ambao utakuwa safarini. Pia, ni muhimu familia yako ijue namna ya kuwasiliana nawe endapo hali za dharura zitatokea.

      [Hisani]

      Taken from the United Behavioral Health Web site

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki